Na Mwandishi wetu
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi
ya Ulinzi na Usalama, Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Mkuu wa Majeshi ya
Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange salamu za rambirambi kuomboleza kifo
cha Luteni Kanali (mst) Adam Hussein Mwandu Makwaia, aliyekuwa mpambe wa
Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na Rais Ali Hassan
Mwinyi.
Rais Kikwete alielezea majonzi na masikitiko yake kufua kifo cha Makwaia
kilichotokea Jumanne, ya Septemba 4, mwaka huu katika Hospitali ya
Jeshi ya Lugalo mjini Dar es Salaam.
“Katika miaka yote ya utumishi wa Jeshi na utumishi wa umma, Luteni
Kanali Makwaia alikuwa mwadilifu na mwaminifu kwa nchi yake, alikuwa na
weledi wa kiwango cha juu katika taaluma yake ya kijeshi na alikuwa
mtiifu kwa viongozi wake,” alisema Rais Kikwete.
Luteni Kanali (mst) Makwaia alijiunga na Jeshi Machi 24, mwaka 1974, na
alilitumikia kwa miaka 23 na miezi tisa kabla ya kustaafu.
Alikuwa Msaidizi wa mpambe wa Rais kati ya mwaka 1978 na 1981 na kuwa mpambe wa Rais kwa miaka sita hadi 1987. Amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 62.
Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada awasili nchini kwa ziara ya
Kikazi
-
Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Canada Mhe. Randeep Sarai amewasili
nchini kwa ziara ya kikazi ya siku Tatu.
Mhe. Sarai anatarajiwa kutembelea miradi m...
26 minutes ago
No comments:
Post a Comment