Habari za Punde

NIDA kuanza usajili vitambulisho vya taifa Okt.10




Na Mwantanga Ame
MAMLAKA ya vitambulisho vya Taifa Tanzania (NIDA), inatarajia kuanza zoezi la usajili kwa wananchi wa Zanzibar Oktoba 10 mwaka huu.

Mkugenzi wa NIDA-Zanzibar, Vuai Mussa Vuai, aliyasema hayo jana wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu zoezi hilo litavyoweza kufanyika.

Mkurugenzi huyo alisema wananchi wote watasajiliwa   ili kupata vitambulisho hivyo, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sheria ya nchi ambayo inawataka wananchi wote kuwa na vitambulisho hivyo.

Alisema zoezi hilo litaanzaa kufanyika katika Mkoa wa Kusini Unguja katika wilaya Kusini  ambapo litachukua kipindi cha wiki mbili kuanzia Oktoba 15 hadi Novemba  26.


Wananchi wa wilaya ya Kati wataanza kusajiliwa kuanzia Oktoba 29  hadi Novemba 9, mwaka huu na wilaya ya Magharibi zoezi hilo litaanza Novemba 12 hadi 23.

Wilaya ya Mjini zoezi litaanza Novemba 26 hadi Disemba 7, mwaka huu na baadae linatarajiwa kuhamia katika wilaya ya Kaskazini ‘B’ ambapo wananchi wa sehemu hiyo wataanza kusajiliwa Disemba 10 hadi 21, mwaka huu na wilaya ya kaskazini ‘A’ watasajiliwa kuanzia Januari 4, 2013.

Alisema wilaya za Pemba wananchi wataanza kuzajiliwa kuanzia Januari 7 hadi 18,  mwakani  na Micheweni ni kuanzia Januari 21, hadi Febuari 2, Wete zoezi litaanza Febuari 4 hadi Febuari 15 wakati  Chake Chake litaanza Febuari 18 hadi Machi 1 mwaka huo.

Alisema vitambulisho hivyo vinatarajiwa kutolewa kwa mfumo wa makundi matatu ambapo utawahusisha  wananchi, wageni na wakimbizi.

Alisema  mtu amabaye atakuwa amehukumiwa adhabu ya kifo, punguwani wa akili kwa mujibu wa sheria hiyo hatasajiliwa.

Alisma katika zoezi hilo wananchi watapaswa kutoa ushirikiano kuweza kulifanikisha na kuacha kuwashirikisha wageni kwa njia za siri jambo amabalo likibainika wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

Alisema searikali imeamua kuanzisha zoezi hilo kwa dhamira ya  kuwatambua watu wanaoishi nchini kwa sasa kwani kumeonekana utambuzi huo haupo jambo ambalo limekuwa likiisababihia serikali kupata hasara.

Alisema vitambulisho hivyo vitaweza kusaidia Bodi ya Mikopo ya Wanafuzi wa Elimu ya Juu kuwatambua wanafunzi wanaostahili kupatiwa mikopo kutokana na hivi sasa kuonekana kuwapo ugumu wa urudishaji mikopo hiyo.

Alisema tatizo la kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu vinavyofanywa na raia wa nchi jirani na wafungwa waliomaliza adhabu zao au wanaoachiwa huru kwa msamaha wa rais hivi sasa umekuwa mgumu kutokana na kushindwa kutambuliwa.

Alisema tatizo la kuongezeka kwa mrundikano wa wafungwa katika magereza kutokana na kutokuwapo udhibiti wa wafungwa wa kifungo cha nje nalo linahitaji kupatiwa ufumbuzi baada ya vitambulisho hivyo vitapoanza kutumuika.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.