Na
Jumbe Ismailly,Singida
CHAMA
cha watafiti na wachimbaji wadogo wa madini (SIREMA) mkoa wa Singida kimesema
endapo serikali itaendelea na msimamo wake wa kupandisha gharama za kulipia
viwanja vya uchimbaji madini kuna hatari ya wachimbaji wadogo 900,000
wanaotegemea kujipatia kipato chao kupitia shughuli za madini watakuwa
wamepoteza ajira zao.
Katibu
Mkuu wa SIREMA mkoa wa Singida, alitoa kauli hiyo wakati akitoa tamko kwa
waandishi wa habari kuhusu kupinga kupanda gharama za kulipia viwanja vya
uchimbaji madini pamoja na shughuli zinginezo zinazohusu madini.
Katibu
Mkuu huyo, alisema tamko hilo
limetolewa na kikao cha kamati tendaji ya chama hicho kilichokutana kwenye
ofisi zake zilizopo mjini hapa.
“Sisi
wachimbaji wadogo wa madini mkoa wa Singida kupitia kamati ya Tendaji ya chama
tumelazimika kutoa tamko letu kuhusu kupanda gharama za ulipiaji wa viwanja vya
kuchimba madini na gharama zingine zihusuzo na shughuli zetu,” alisisitiza Marando.
Aidha Katibu huyo alifafanua kuwa serikali kupitia
wizara ya nishati na madini ilipandisha gharama hizo mwaka 2010 na hatimaye
kupandisha tena gharama hizo Julai,27,mwaka huu na kwamba kupanda huko
kumefanyika bila kufanya utafiti wa kina kama
zinalipa au la.
Aliweka
bayana kwamba kupanda kwa gharama hizo kunalenga zaidi kuondoa Watanzania
wazalendo wanaojihusisha na shughuli za uchimbaji madini na kuwanyang’anya
maeneo ya uchimbaji mdogo ili kuwapa wageni ambao wao hupewa misaada na nchi
zao.
Kwa
upande wake mmoja ya wachimbaji wadogo,Mather
Kayaga, alifafanua kuwa kwenye sekta ya madini wanawake ni asilimia 25 tu ya
wachimbaji wote na kwamba hawachimbi kibiashara bali hufanya kazi hiyo kwa
lengo la kuisaidia familia zao.
“Mimi
binafsi nimepatwa na mshituko mkubwa sana baada ya kusikia ongezeko la ada hiyo
na siamini kabisa kama nitaweza kulipa kiwango hicho kikubwa kiasi hicho,”alisema
Naye
Julius Madembwe alisisitiza kuwa wachimbaji wadogo ndio wenye historia ya
madini na wachimbaji wakubwa hupata kwa kupitia kwao.
Kwa
upande wake Philip Mwembe alisema imekuwa kawaida ya serikali kutoa ahadi na
kushindwa kuzitekeleza na hivyo kutumia fursa hiyo kuikumbusha ahadi
iliyotolewa kwenye kikaoa cha Bunge la bajeti la 2012/2013 kwamba kuna shilingi
bilioni tisa kwa ajili ya wachimbaji wadogo,nao wanufaike nazo badala ya
kuendelea kuzisikia kwa wengine wanaopata upendeleo huo.
No comments:
Post a Comment