Na Madina Issa
JUMUIYA ya Wazazi Mkoa wa mjini Magharibi
imemchagua Ali Othman Said kuwa
Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo baada ya kupata kura 71.
Mwengine waliochaguliwa ni wajumbe watatu wa baraza
la Mkoa ambao ni Mohamed Said Dimwa, Najma Mutaza Giga na Sufiani Ramadhan
Khamis.
Aliyepata nafasi ya kuwakilisha baraza kuu taifa
pamoja na mkutano mkuu taifa CCM ni Saleh Said Abdallah ambae amepata kura 67.
Mjumbe mmoja anaewakilisha Halmashauri Kuu na
mkutano mkuu Mkoa ni Nassibu Mohamed Haji ambae amepata kura 55, mjumbe mmoja
wa baraza kuu Wilaya ya Aman ni Mwalim Haji Ameir aliyepata kura 55.
Wengine ni mjumbe wa baraza kuu Wilaya ya mjini
ambao ni Maulid Suleiman Juma, mjumbe mmoja atakae wakilisha UWT Mkoa ambae ni
Hakiba Khamis, pamoja na mjumbe mmoja wa kuwakilisha vijana Hassan Jecha aliepata
kura 88.
Wakitoa neno la shukurani viongozi hao waliahidi
kuwa watakitetea chama na kukilinda kwa maslahi ya wote na sio kwa mtu mmoja.
Akifungua
mkutano huo, Katibu wa Idara ya Oganaizesheni ya CCM, Asha Abdallah Juma aliwataka
wajumbe kuchagua viongozi bora na sio bora viongozi ili kuweza kukipa ushindi
chama cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu 2015.
Alisema endapo wanajumuiya hao watakachagua
viongozi waliokuwa makini, imara na waaminifu wataweza kukivusha chama hicho
katika chaguzi mbalimbali zinazokuja.
Katibu huyo alisema CCM ndio chama pekee
kilichokuwa imara na chenye demokrasia makini ya kuongoza hivyo wasisite
kukipatia viongozi waliokuwa imara kwa maslahi ya wananchi wote.
"Katika nchi hii chama chenye demokrasia
makini ya kuongoza ni CCM mimi sioni sababu ya kukibeza chama hichi, kwani mtu
yeyote anayekibeza nahisi ameishiwa sera za kufanya," alisema Asha.
Alisema kuna baadhi ya wapinzani wanasema CCMkimepoteza
muelekeo, lakini alisema wanasiasa hao wanajidanganya na wanawambia uongo
wafuasi wao.
Hata hivyo aliwasihi watakaochaguliwa katika nafasi
hizo wawe waadilifu na waaminifu katika utendaji wa kazi zao.
Akizungumzia mchakato wa katiba aliwasihi wanajumuiya
hao kutoa maoni yao
yaliyokuwa imara na sahihi yatakayoendelea kuudumisha muungano.
Nae Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Magharibi,
Yussuf Mohamed Yussuf aliwahimiza
wanaCCM kulinda chama chao ili kuweza kukisongesha mbele katika gurudumu
la siasa.
No comments:
Post a Comment