Na Othman Khamis, OMPR
SERIKALI
inakusudia kujiandaa mapema na maandalizi makubwa ya maadhimisho ya sherehe za
Mapinduzi ya Zanzibar
ya mwaka 1964 kutimia miaka 50 ambazo zitatarajiwa kuwa za kihistoria.
Mwenyekiti wa
Kamati ya Sherehe na maadhimisho ya Kitaifa Zanzibar ambae pia ni Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif alitoa kauli hiyo wakati wa tafrija
maalum ya kupongezana na kuelewana kwa maafisa wa gwaride iliyofanyika hoteli
ya Bwawani mjini Zanzibar.
Balozi Seif
alisema ili kufanikisha azma hiyo ya serikali,mashirika, taasisi za kijamii na
watu binafsi wanapaswa kuanza na maandalizi mapema kwa lengo la kupata ufanisi
unaokusudiwa.
Alisema serikali
itaendelea kuunga mkono vikosi vya ulinzi na usalama kwa kuwa ndivyo vyenye
nafasi kubwa ya kusherehesha.
Alieleza kuwa
vikosi vya ulinzi na usalama vimefanya kazi kubwa mwaka huu iliyopelekea
kufurahisha na kupendezesha maadhimisho hayo.
Alisema mapinduzi
ya Zanzibar ya
mwaka 1964 yameleta faida kubwa kwa wananchi waliowengi na kuwafanya kuwa
mstari wa mbele katika maendeleo na kusherehekea sherehe hizo.
Akimkaribisha
Balozi Seif, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais , Mohammed Aboud alisema
majeshi ya ulinzi yameonesha umahiri mkubwa katika kuchapa gwaride.
Mapema kamanda wa
Brigedi 101 Zanzibar, Brigedia Jenerali, Sharif Sheikh ameahidi vikosi vya
ulinzi na usalama vitaendelea kushirikiana na serikali katika kuona maandalizi
ya maadhimisho miaka 50 ya mapinduzi
yanafanikiwa kwa ufanisi zaidi.
mapinduzi gani hayo yalitoa roho za watu wasio na hatia? ndio maana mmelaaniwa mpaka leo si umeme wala maji mmeweza kusambaza ktk visiwa ukubwa wake hauzidi mkoa wowote kule bara kwa mabasha zenu , mambo muhimu yankushindeni mnafikiria kusheherekea , hospitali na shule zote mahututi , wendawazimu waliovaa kistaarabu ,
ReplyDelete