Habari za Punde

Uzinduzi wa Rasimu ya Katiba kuoneshwa 'live'

Ili kuwafikia wananchi wengi, uzinduzi wa Rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania utakaofanyika kesho, Jumatatu, Juni 3, 2013, kuanzia saa 8:00 mchana katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam utarushwa moja kwa moja na vituo vya TBC1, TBC Taifa, ITV, Star TV, Channel Ten, ZBC TV na ZBC Redio. Wadau hawa wamekubali kufanya hivyo baada ya kuombwa.
Uzinduzi huo utarushwa moja kwa moja na vituo hivyo kuanzia saa 8:00 mchana.
Rasimu hiyo ya Katiba imetokana na maoni ya wananchi, viongozi na makundi mbalimbali waliyowasilisha kwa Tume kupitia njia mbalimbali zikiwemo mikutano, barua pepe, ujumbe mfupi wa simu za mikononi (sms) na nyinginezo.


--
Omega S. Ngole,
Principal Information Officer,
Constitutional Review Commission (Tanzania),
PO Box 1681,
Dar es Salaam,
Facebook:www.facebook.com/people/Omega-Ngole
Twitter: https://twitter.com/OmegaNgole

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.