Na
Mwandishi wetu
IKULU
imeelezea kusikitishwa, kufadhaishwa na kusononeshwa, kuhusu madai kwamba
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa Aprili 24, 1964 si halali, kwa sababu
hakuna hati ya Muungano.
Akizungumza
na waandishi wa habari Ikulu jana, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue,
alisema kauli hizo sio tu zimeisononesha serikali lakini Watanzania pia.
Alisema
kamwe Ikulu haikuamini kama hali ingekuwa
hivyo kwa baadhi ya Watanzania kuhoji uhalali wa muungano miaka 50 baada ya
kuasisiwa kwake.
Alisema
hati ya makubaliano ya Muungano ipo na inahifadhiwa kama
mboni ya jicho katika maeneo maalum ili isiharibike au kupotea kwa sababu ni
nyaraka nyeti na kwa hali ya kawaida huwa hazitolewi.
Hata
hivyo, alisema kwa maagizo ya Rais Jakaya Kikwete, wameamua kuitoa hati halisi
ya Muungano huo yenye saini za waasisi wake na kwamba saini zao hazikuhushiwa.
Aidha
alisema hati hiyo itawasilishwa tu mbele ya bunge maalum la katiba, iwapo
serikali itaombwa na Mwenyekiti wa bunge maalum la katiba kufanya hivyo.
Alisema
ili kuhakikisha Watanzania wanapata fursa ya kuisoma, alisema serikali
itaziweka nakala za mkataba huo katika
makumbusho ya taifa.
Balozi
Sefue alitumia fursa hiyo kuwaonesha waandishi wa habari nakala halisi ya
Muungano huo na nakala zake kuzigawa kwa waandishi wa habari.
Alisema
mbali ya hati hiyo, hati nyengine zilihifadhiwa katika mazingira nyeti ni hati
ya uhuru wa Tanganyika
na hati ya Tangayika kuwa Jamhuri na kukiri kwamba hawapendi kuionesha.
No comments:
Post a Comment