Na
Mwantanga Ame, Dodoma
BAADA
ya kuzuka utata mkubwa juu ya hati ya Muungano kama ipo ama haipo, Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais, Mahusiano na Utaribu, Steven Wasirra, amekubali yaishe baada ya
kusema hati ya Muungano ipo na ipo salama katika miaka 50 ya Muungano.
Akiwasilisha
ripoti ya kamati namba sita, Wasira
alisema hati hiyo itawasilishwa kwa Mwenyekiti wa bunge, Samuel Sitta,
katika kipindi cha siku mbili zijazo.
“Kwa
niaba ya dola ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nitawasilisha hati ya
makubaliano ya Muungano yenye saini marehemu Abeid Amani Karume na Mwalimu
Julius Nyerere,” alisema Wasira na kuamsha nderemo.
Wakichangia
mjadala, mjumbe Moses Machale, alionesha kushangazwa na serikali kutangaza kuwa
na hati ya Muungano katika kipindi
kifupi kiasi hicho na kuhoji uhalali wake.
Mohammed
Chombo, alisema Muungano wa Tanganyika
na Zanzibar una maadui ndani na nje ya Tanzania na ndani ya bunge hilo .
Alisema
wenye nia mbaya wanataka kuvunja Muungano na kuifanya Tanzania isiwe na amani
na kusababisha vurugu, ubaguzi na chuki.
Bunge
lilichangamka zaidi pale mjumbe Asha Bakari, alipohoji sababu ya watu kuanza
kudai hati ya muungano wakati Zanzibar
imeunda Serikali ya Umoja wa kitaifa bila ya hata kuwapo mkataba uliofikiwa na
kwamba ni vyema wanaodai hati ya Muungano wangelianza kudai mkataba huo.
Nae
Dk. Khamis Kigangwala, alisema kuna tatizo kubwa kwenye takwimu za Tume ya Jaji
Warioba, kwani takwimu alizokuja nazo ni za watu wa mikoa miwili.
Kwa
upande wake Zakia Meghji, alisema yeye binafsi alikuwa hana wasiwasi wa kutokuwepo
hati ya Muungano kwa sababu kuna machapisho mengi yanayothibitisha kuwepo hati hiyo.
Alisema
kinachoonekana kuna watu walikuwa na dhamira ya kuifanya Tanzania
isifikie hapo ilipo.
Wasira
akizungumzia juu ya suala la mfumo wa serikali mbili, alisema si vyema kwa wajumbe wa bunge hilo kutumia nafasi zao
kuwadanganya wananchi juu ya mfumo huo.
Alisema
Tume ya Warioba, imeshindwa kufanya uchambuzi wa kina katika kuingiza sehemu
kubwa ya mapato ya serikali ya Tanzania kuwa jambo la Muungano, na balada yake imeangalia
baadhi ya wizara zinazoshughughulikia mambo ya Muungano.
Alisema
mfumo wa serikali mbili una uwezo mkubwa wa kutanua biashara na masoko kwa mtu
mmoja mmoja na waliowa chache bila ya kuwepo masharti ya uhamiaji na
utapofanyiwa marekebisho utaweza kuondoa kero na manung’uniko yaliyopo sasa.
Alisema
licha ya ubishi unaoendelea kutokea juu ya suala la gharama za uendeshaji wa
serikali tatu kuna uwezekano mkubwa
serikali ya shirikisho ikaanguka, na kwamba hata Prof. Ibrahim Lipumba,
amelikiiri hilo
katika moja ya mada zake.
Alisema
hali hiyo pia inajionesha kwa upande wa Tanzania Bara ambako kati ya watu
16,321 waliochangia hoja ya Muungano wa serikali tatu ni 8682 kutoka mkoa wa
Kigoma ambao ni sawa na asilimia 52 na waliobakia kati 7,000 walitokea mikoa mengine ikiwemo Tabora,
lakini anashangaa kuona tume kusema watu wengi wanataka muungano wa serikali
tatu.
Alisema
kama tume inaona ipo haja ya kuwa na mfumo huo wa serikali tatu basi
ililazimika kwanza kupendekeza kuvunjika Muungano.
Akizungumzia
juu ya maoni ya wachache, alisema sehemu kubwa ya maoni ya wajumbe hao
walikubaliana na maoni ya Tume ya katiba.
Alisema
katika maoni yao, waliorodhesha mambo manane ambayo yanaonekana kuwa na
matatizo ya kisheria juu Muungano ikiwemo suala la kutunga sheria, msingi wa
Muungano na utaifa, mgawanyo wa mambo yasiokuwa ya Muungano, bajeti na mambo ya
fedha za muungano, udhaifu wa jumla wa mambo ya Muungano na rasilimali za
Muungano.
Mjadala
huo ulionekana kugeuka mwiba baada ya kuwepo msisitizo wa kuletwa hati ya Muungano.
Asha
Mtwangwi alisema kinachoonekana baadhi ya wajumbe wanashindwa kufanya utafiti
kabla ya kusema kwani wanasahau kuwa nchi haina uwezo wa kuhesabika kuwa nchi
kama haina muhimili huku Amon Mpanji akisema bado Tanzania inahitaji amani katika
mfumo wa serikali mbili.
No comments:
Post a Comment