Habari za Punde

Mvua balaa Dar.

Na Fatuma Kitima, DSM
IDADI ya watu waliokufa kutokana na mvua imeongezeka kufikia 11,  baada ya mtu mmoja mkazi wa Kimara, Suka Golan, kukutwa akiwa amekufa katika eneo la Unyamwezini kati ya Makoka na Kimara.

Kifo hicho kinafanya idadi ya waliokufa kufikia 11 kutokana na mvua hizo.

Taarifa kutoka kwa shuhuda wa tukio, Aman Shaban, alisema maiti ilionekana eneo hilo majira ya saa 12:00 jana, ambapo mwili wake ulikutikana ukimwa umekwama kwenye miti.

Alisema baada ya kuona mwili huo, taarifa  ilitolewa kwa jeshi la  polisi ambapo baada ya muda mfupi walifika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu.

Mbali ya vifo, mvua hizo zimesababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu ambapo daraja la Makoka liliopo mpakani kwa Kinondoni na Ilala limebomoka na kusababisha  huduma za usafiri kukwama.


Hali hiyo inasababisha wananchi kulipa shilingi 500 kwa vijana waliopiga kambi katika daraja hilo kwa ajili ya kuwavusha watu.

Katika tukio jingine magari takribani 35 ya kampuni ya usambazaji mabomba ya gesi yamesombwa na maji katika eneo la Mzinga Mbagala jijini Dar es Salaam.

Taarifa kutoka kwa mashuhuda kutoka eneo la tukio, zilisema magari hayo yanayomilikiwa na Wachina, yalikokotwa na maji wakati yakiwa yameegeshwa.

Wakati huohuo, Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Dar es Salaam, imetoa taarifa kuhusu madhara ya mvua zinazoendelea kunyesha.

Taarifa ya kamati hiyo ilisema mvua hizo zimesababisha vifo, nyumba kubomoka huku nyumba nyingine zikiwa bado zimezingirwa ma maji.

Madaraja takribani 11 yamesombwa na maji na mengine kuvunjika  huku mengine yakiwa yamefunikwa kabisa likiwemo daraja la mto Mpiji  mpakani wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani katika barabara iendayo Bagamoyo ambalo kingo zake upande wa Dar es Salaam zimesombwa na maji na kusababisha mawasiliano kati ya Bagamoyo na Dar es Salaam kukatika.

Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib, ametembelea eneo hilo kujionea uharibifu mkubwa uliosababishwa na mvua.

Katika maeneo ya Mlandizi, kumekuwa na foleni kubwa ya magari ya mikoani iliyosababishwa na mafuriko katika mtu Ruvu.


Aidha, daraja la Visiga liliopo kilimoita 35 kabla ya kuingilia Mlandizi limetitia na malori hayaruhusiwi kupita na kusababisha mawasiliano ya barabara kati ya Mlandizi na Chalinze kukatika.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.