Habari za Punde

Sekta ya Utalii inakabiliwa na ukosefu wa utoaji huduma bora


 Sekta ya utalii Tanzania inakabiliwa na ukosefu wa utoaji huduma bora tatizo linalochangia upungufu wa watalii wanaotembelea nchini ikilinganishwa na nchi za jirani.

Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi inayotoa huduma za Utalii Tanzania ya Travel port,  Elisaph Mathew alisema miongoni mwa matatizo hayo ni gharama na watendaji wasiokuwa na ujuzi hali aliyodai imesababisha malamiko mengi ya wageni na kupunguza mapato.

Akizungumza katika hafla ya utoaji vyeti kwa wahitimu wa mafunzo ya utoaji wa huduma za sekta hiyo kwa njia ya Electronic amewataka wadau wa sekta hiyo kuacha kufundisha watendaji wao kiholela ili kupata watendaji watakaofanya kazi kwa ufanisi

Nae Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya kitalii ya Zenith Salim Mohamed Suleiman amesema Zanzibar imepata nafasi nzuri katika kukuza sekta ya utalii na kufikia viwango vya kimataifa.

Mafunzo hayo utoaji wa huduma kwa njia ya elekrtonic ni ya kwanza zanzibar yametolewa kupitia kampuni ya zenith kwa ushirikiano na kampuni ya Travel port yenye matawi zaidi ya mia na hamsini duniani

1 comment:

  1. HAO NI GALILEO BWANA.... WANAONGOZA KWA UBORA WA HUDUMA ZAO.
    NA KAMA MTU ANAHITAJ KUFUNGUA KAMBUNI YA TRAVEL (AIR TICKTING) AWAFUATAE...
    Thanks for a good news.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.