Na
Anna Nkinda, Maelezo
WANAFUNZI
wa kike wa vyuo vikuu nchini wametakiwa kujitambua na kufahamu wajibu wao kwa
jamii inayowazunguka na kujiepusha na vishawishi vikiwemo vya ngono na kujikomboa kifikra, kiutamaduni na kiuchumi.
Pia
wametakiwa kujua thamani yao na kuepuka kutumiwa
vibaya na kushinda majaribu ya watu wanaotaka kuivuruga safari yao ya maisha.
Wito
huo umetolewa na mke wa Rais, mama Salma Kikwete, wakati akizungumza na wanafunzi
wa kike wa vyuo vikuu waliohudhuria kongamano la mustakabali wa mtoto wa kike
katika mazingira ya sasa lililofanyika katika ukumbi wa Chimwaga uliopo Chuo Kikuu
cha Dodoma
(UDOM).
Mama
Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA),
alisema kila mtu amepewa karama za kumuwezesha kufikia wito wa kutimiza ndoto
zake ili kuweza kufanikisha hayo hana budi kujitambua, kuvitunza na kuvilea
vipawa na karama zake na kuyakubali mapungufu yake katika kutimiza azma zake.
“Kataa
kabisa mawazo ya kukatisha tamaa kwani hofu kama ilivyo furaha huuambukiza,
jaribu kuwaepuka marafiki wenye mawazo ya kukatisha tamaa kwani hao ndiyo
maadui wakubwa wa maisha yako na wa kukukwamisha kufikia malengo yako,”
alisema.
“Kuna
wakati inawezekana ukawa na hamu ya kuona malengo yako yanatimia mara moja
ukweli ni kwamba hamu yako ya kuleta mabadiliko ya haraka yanaweza kukuletea
madhara makubwa kuliko faida na hapa ndipo mabinti wengi huharibikiwa kwa
sababu wanakosa subira na hivyo kufanya mambo yao kinyume na utaratibu na
malengo,” aliasa.
Aliwahimiza
wanafunzi hao kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika vyuo vyao kwa
kufanya hivyo watajiwekea mazingira mazuri ya kuwa viongozi wa baadaye pindi
watakapomaliza masomo.
“Wanawake tuna nafasi ya pekee ya uongozi
kwani sisi ndio wazazi na walezi tunaokabiliwa na changamoto nyingi, hivyo basi
sisi tuna mchango wa pekee katika kutatua changamoto hizo lakini tutaweza
kufanya hivyo kama tutaingia katika ngazi ya maamuzi jambo la muhimu ni
kupendana na kuungana katika mambo ya maendeleo kwa ajili ya maslahi yetu kama
wanawake,” alisema.
Akisoma
risala ya wanafunzi hao, mwakilishi wa wanafunzi, Hamida Salum, alisema katika
maisha suala la kujitambua ni la muhimu kwakuwa wanafunzi wengi wa elimu ya juu
wanasoma bila ya kuwa na malengo hali inayosababishwa na kutojitambua.
“Changamoto zinazomkabili mtoto wa kike ni
nyingi baadhi ni kutokuwa na elimu ya
afya ya uzazi na jinsia jambo ambalo limesababisha wasichana wengi kujihusisha
katika mahusiano yasiyo salama, dhana potofu ambayo imejengeka katika jamii
kwamba wanawake hawawezi kuwa viongozi kiasi cha kuwaathiri hata watoto wa kike
wenye uwezo wa kuongoza,” alisema.
Alisema
sera nyingi za nchi zimemsahau mtoto wa kike katika mambo yanayomuhusu na hivyo
kumfanya aonekane duni kwenye jamii.
Wanafunzi
hao pia waliiomba serikali itazame upya sera ya utoaji wa mikopo kwa wanafunzi
wa elimu ya juu hasa wasichana kwakuwawengi wao hawakidhi vigezo vya kupewa
mikopo na wanahitaji kusoma hivyo wanafunzi wanaotoka katika familia zenye
uwezo duni kiuchumi kushindwa kuendelea na masomo.
Kongamano
hilo la siku moja liliandaliwa na Chuo
kikuu cha Dodoma na kuhudhuriwa na wanafunzi wa kike zaidi ya 3000 kutoka Chuo
cha Elimu ya Biashara (CBE), Chuo kikuu cha Mt. John, Chuo kikuu Mzumbe, Chuo
cha Mipango, Chuo cha Hombolo, Chuo cha Madini na Shule ya sekondari Dodoma.
No comments:
Post a Comment