Habari za Punde

UKAWA watahadharishwa kutoharibu mjadala wa katiba

Na Mwantanga Ame, Singida
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, amesema hawatakubali kuona Umoja wa Katiba ya  Wananchi (UKAWA), unauchafua awamu ya pili ya mjadala wa kupatikana katiba mpya, kwani kamati 12 za bunge zimemaliza kazi zake vizuri.

Aliysema hayo wakati akiwahutubia wanachama wa CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Chiuyu, wilaya ya Manyoni mkoaniSingida.

Balozi Seif, ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, alisema wanalazimika kutoa tahadhari hiyo kwa vile tayari kuna taarifa kwamba umoja huo huenda ukarudi bungeni baada ya kuzungumza na Rais Kikwete.

Alisema nafasi yao ya kurudi isiwe sababu ya kuchafua awamu ya pili ya mjadala huo.

Alisma CCM itaendelea na msimamo wake wa kutetea mfumo wa serikali mbili kwa sababu wananchi wameshaelewa madhara ya mfumo wa serikali tatu.

Alisema inashangaza kuona baadhi ya watu kudai wajumbe wa CCM, hawajadili rasimu ya Jaji Warioba, wakati taratibu zinawaruhusu wajumbe kurekebisha palipokosewa.


Aidha alisema madai kuwa katiba inayotungwa ni ya CCM hayana ukweli kwa sababu wajumbe wengine kutoka kundi la 201 wanashiriki kujadili.


Alisema nia ya serikali ni kuona Tanzania inapata katiba iliyo bora na itakayowaunganisha wananchi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.