Na Kija Elias, Tanga
Mkaguzi wa skuli za sekondari manispaa
ya Moshi, mkoani Kilimanjaro, Mtenguzi Kidyamakuo, ametangaza nia ya kugombea ubunge
jimbo la Handeni mkoani Tanga, katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.
Jimbo hilo kwa sasa
linashikiliwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdhalla Kigoda.
Alisema atagombea nafasi hiyo kwa
tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA).
Alisema amefikia huo uamuzi kwa
lengo la kuharakisha masuala ya kimaendeleo ambayo amedai yanasuasua.
“Jimbo hili limekuwa na wabunge
mbalimbali kwa zaidi ya miaka 20 sasa lakini hakuna maendeleo ya haja ambayo
wananchi wake wanaweza kujivunia,” alisema.
Alisema moja wapo ya changamoto
ambazo atalishughulikia ni pamoja na miundombinu ya barabara na maji ambayo
alisema zimekuwa zikikwamisha wananchi katika juhudi zao za kujikwamua
kiuchumi.
“Ukija kwa huduma za afya
wananchi wa jimbo hili wanalazimika kutembea zaidi kilomita 30 kufuatialia
huduma hizo huku waathirika wakubwa wakiwa ni watoto, wanawake na wazee,”
aliongeza.
Alivitaja baadhi ya vijiji
ambavyo vinakabiliwa na changamoto hizo kuwa ni Kwa Magoma, Msente, Tilibe,
Muumbiri, Mzindu, Kwa Mkono na Kwedikwazu.
No comments:
Post a Comment