Habari za Punde

Mahafali ya 21 ya Chuo cha Taaluma ya Sayansi ya Afya Zanzibar.

Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Taaluma za Afya Zanzibar Dkt. Abdalla Ismail Kanduru akitoa tamko la kuwatunuku stashahada wahitimu wa Chuo hicho katika Mahafali ya 21 yalifanyika Mbweni.
 Wahitimu wa Chuo cha Taaluma za Afya  Zanzibar wakila kiapo cha utiifu mbele ya mgeni rasmi Balozi Seif Ali Iddi katika mahafali ya 21 yaliyofanyika chuoni Mbweni.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na wahitimu wa Chuo cha Taaluma za Sayansi za Afya Zanzibar katika Mahafali ya 21 yaliyofanyika Chuoni Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar. Wa kwanza (kulia) ni Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman na wa kwanza (kushoto) Mwenyekiti wa Baraza la chuo hicho Dkt. Abdalla Ismail Kanduru

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimtunuku  zawadi Mhitimu Leila Ali kwa kuwa miongoni mwa wanafunzi  waliofanya vizuri zaidi katika mahafali ya Chuo cha Taaluma za Afya Mbweni Zanzibar.
Wahitimu wa fani mbali mbali wa Chuo hicho wakimsikiliza mgeni rasmi (hayupo pichani) baada ya kuwatunuku stashahada katika mahafali ya 21.
Wageni waalikwa walioshiriki mahafali ya 21 ya Chuo cha Taaluma za Afya Zanzibar wakifuatilia maadhimisho  hayo yaliyofanyika Chuoni, Mbweni.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.