Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi, akizungumza muda mfupi kabla wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hawajapigia kura ya kutaka vikwazo vya kiuchumi, kibiashara na kifedha ambavyo Marekani imeiwekea Cuba viondolowe. Nchi 188 zilipiga kura ya ndiyo, mbili zilipiga kura ya hapana na tatu zilipiga kura ya kutofungamana na upande wowote
Na Mwandishi Maalum , New York
Kwa mwaka wa
23 sasa hapo jana (
Jumanne ) Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wamepigia kura Azimio linaloitaka Marekani iondoe vikwazo vya kiuchumi, kibiashara na kifedha dhidi ya Cuba.
Katika upigaji kura
huo , nchi 188
ikiwamo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
zilipiga kura ya ndiyo Azimio
hilo ambalo liliwasilishwa mbele ya
wajumbe na Waziri wa Mamb ya Nje wa
Cuba, Bw. Bruno Rodriquez Parrilla
Marekani na
Israel zenyewe zilipiga kura ya hapana, huku
Micronesia, Marshall Islands na Palau
wakipiga kura ya kutoegemea upande wowote ( abstentions).
Akizungumza
kabla ya upigaji kura huo
kufanyika, Naibu Mwakilishi wa
Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Balozi Ramadhan Mwinyi aliungana na wazungumzaji wengine katika kuitaka Marekani na Cuba
kumaliza tofauti zao za
kidiplomasia ili waweze kushirikiana na nchi nyingine katika kuzitafutia ufumbuzi
changamoto mbalimbali zinazomkabili mwanadamu.
Akasema dunia
imeshuhudia namna gani mataifa mengi yalivyojitoa muhanga zikiwamo Cuba na Marekani ambapo
wamepeleka wataalamu wao wa afya, wanajeshi na
vifaa ili kuukabili ugonjwa wa Ebola katika nchi za
Liberia, Sierra Leone na Guinea
ambazo zimeathirika vibaya kwa ugonjwa
huu.
Akasisitiza kuwa mlipuko huo wa Ebola umethihirisha namna gani mataifa yanavyoweza
kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja na kwamba mataifa yanatakiwa kujenga
mshikamano imara dhidi ya maadui
wa binadamu na siyo kupingana wenyewe kwa wenyewe.
Balozi Mwinyi
akaongeza kuwa Tanzania ambayo ni
nchi rafiki kwa Marekani na Cuba, kwa mara nyingine inasikitika kusimama na
kuzungumzia kuhusu vikwazo hivyo ambavyo licha ya maazimio mengi
kupitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Bado vikwazo vinaendelea.
Vile vile
Balozi Mwinyi amesema hali ya
kuendelea kwa vikwazo hivyo kunasikitisha kutokana na sababu kuu mbili za
msingi. Kwanza kuchelewa kulipatia ufumbuzi
tatizo hilo kunadhoofisha hadhi ya Umoja
wa Mataifa, chombo chenye dhamana ya kuhifadhi Amani na usalama wa kimataifa, kuhuisha haki za binadamu, uchumi na ustawi
wa wote.
Akasema inaposhindikana kutekelezwa kwa maazimio
yanayopitishwa na Baraza Kuu la Umoja
wa Mataifa ni kushindwa kwa wanachama
wote.
Sababu ya pili ambayo amesema inasikitisha ni
kuona kuwa Nchi ambayo ilikuwa mwazilishi wa Umoja wa Mataifa (
Marekani) inaendelea kupuuza wito ambao umekuwa ukitolewa mara kwa mara, wito
unaotolewa wanachama wa Umoja wa Mataifa
wa kutaka kusitishwa mara moja na bila masharti yoyote vikwazo dhidi ya Cuba.
“ Tatizo hili ( vikwazo) linaweza kuwa ni la
kati ya nchi hizo mbili. Lakini kuendelea kwake na muda mrefu kunavuka mipaka ya nchi hizi mbili” akasema Balozi
Mwinyi
No comments:
Post a Comment