Habari za Punde

Saba wafariki wakiiba umeme

Na Kija Elias, Moshi
Watu saba wamefariki dunia mkoani Kilimanjaro, akiwemo mzee mwenye umri wa miaka 83, katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Oktoba mwaka huu, baada ya kunaswa na umeme kutokana na kujiunganishia umeme kinyume cha sheria.
Mzee huyo aliefahamika kwa jina la Thadei Mushi, mkazi wa Otaruni kata ya Kibosho kati, alifariki wakati akijiunganishia umeme kutoka kwenye nyumba ya mtoto wake, baada ya nyumba yake kukatiwa umeme kutokana na kulimbikiza madeni.
Mhandisi Mthibiti wa Mapato wa Shirika la Umeme (TANESCO) mkoa wa Kilimanjaro,  Bakabuje Joseph, alisema kumekuwepo na wizi mkubwa  wa umeme na  miundombinu ya umeme hali iliyoisababishi shirika hasara ya zaidi ya shilingi milioni 110.

 Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, alisema wananchi wengi wamekuwa na tabia ya kujiunganishia umeme kinyume na taratibu jambo ambalo linasababisha wengine kupoteza maisha.
Aidha alisema shirika linahujumiwa kutokana na miundombinu yake kuharibiwa ambapo wezi wamekuwa wakikata waya zenye shaba na kuziuza kama nyuma chakavu.
Aidha, alisema wizi hao wamekuwa wakiiba mavuta ya transfoma hali inayosababisha hasara kubwa kwa shirika.

Naye mtoto wa marehemu, Venance Mushi, alisema kifo cha baba yake, kimesababishwa na hitilafu za umeme wakati akijiunganishia huduma hiyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.