Habari za Punde

Watakiwa kutowatumikisha watoto

Na Zainab Anuwar
Wazazi na walezi wameshauriwa kutowafanya watoto wao vitega uchumi na kuwafanyisha kazi ngumu.

Kauli hiyo imetolewa na Mwalimu Mkuu wa skuli ya msingi Uzini wilaya ya kati, Silima Haji Silima, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi.

Alisema kitendo cha kuwatumikisha watoto na kuwalazimisha kufanya kazi kwa ajili ya kuhudumia familia zao hakikubaliki kwa sababu kinawanyima fursa ya kusoma.

Aidha alisema wazazi wengi katika shehia hiyo wamekuwa na tabia hiyo jambo ambalo husababisha watoto wengi kukatisha skuli na kubakia nyumbani.

Alisema ajira za watoto zinasababishwa na changamoto mbali mbali ikiwemo wazazi kutokuwa na mwamko wa elimu.

Kwa upande wake Mwajuma Makungu Is-haka ambae ni miongoni mwa wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika skuli hiyo, alisema kuna baadhi ya wazazi wanadharau elimu na kuamua kuwatumikisha watoto wao katika kazi za mikono.



Skuli ya Uzini Msingi ina jumla ya wanafunzi 534 ambapo wanaume ni 260 na wanawake 274.      

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.