Na Zainab Anuwar
Mkurugenzi wa Manispaa
Zanzibar, Abedi Juma Ali, wamewataka wafanyabiashara wa soko la kuku Darajani
kufanya shughulia katika hali ya usafi.
Aliyasema hayo wakati akizindua
kifaa cha kuchujia manyoa ya kuku kwa lengo la kuweza kudhibiti utapakaaji wa
manyoa hayo ndani na nje ya soko hilo.
Alisema kifaa hicho kitasaidia
kiwango kiasi kikubwa kulinda mazingira katika soko hilo.
Aidha aliwataka kushirikiana na
manispaa kuhakikisha hali ya usafi inaimarishwa katika soko hilo.
Mwenyekiti wa Glitters
Volunteer Group Zanzibar Cleaning, Mohamed Khamis, alisema manyoa ni mali ambayo hutumika
kutengenezea mambo mbali mbali kama vile nguo pamoja na kutumika kama ni
mbolea.
Hata hivyo, alisema bado soko
la manyoa kwa Zanzibar ni dogo kutokana na idadi ndogo ya kuku wanaochinjwa.
Alisema kifaa hicho kitasaidia
kutunza mazingira ya soko hilo na utapakaaji wa manyoya uliozoeleka katika soko
hilo.
No comments:
Post a Comment