Mwanasheria
Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman akipiga kura leo kwenye ukumbi wa
Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma kupitisha Sura na Ibara za Rasimu ya Katiba
inayopendekezwa.
Mjumbe
wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Yahya Kassim Issa akiomba mwongozo leo Bungeni
kwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta kuhusu kitendo cha
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman kuja kupiga kura na
kukataa baadhi ya Ibara za Rasimu ya Katiba inayopendekezwa wakati alijitoa
kwenye Kamati ya Uandishi ambapo alitakiwa awepo akitetea maslahi ya Zanzibar,
jambo ambalo limewachanganya baadhi ya wajumbe.
Mwanasheria
Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman akisindikizwa kutoka ndani ya
ukumbi wa Bunge Maalum leo mjini Dodoma na Askari Polisi.
Mwanasheria
Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman (mwenye Kaunda suti ya kijivu)
akisindikizwa kutoka nje ya viwanja vya Bunge Maalum la Katiba leo mjini Dodoma
na Askari Polisi mara baada ya kushutumiwa na baadhi ya Wajumbe wa Zanzibar.
Wajumbe
wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Mzee Kingunge Ngombale Mwiru pamoja Waziri wa
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mhe. Dkt. Fenella Mukangara
wakibadilishana mawazo kwenye viwanja vya bunge hilo mjini Dodoma leo.
Waziri
Mkuu wa Tanzania ambaye pia ni mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Mizengo
Pinda akibadilishana mawazo kwenye viwanja vya bunge hilo
mjini Dodoma leo na Mjumbe Wabunge hilo nje jengo la bunge Dodoma.(Picha na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma)
hii kura ya wazi kumbe haiwezekani kuchakachuliwa?, basi bora hata uchaguzi mkuu itumike.
ReplyDeletemasikini CCM muliona mumepaata pale muliposema kura ipigwe ya wazi (watu wataogopa) lakini mungeweka kura ya siri si sasa hivi mungefanya munavyotaka (mungechakachuwa) lakini mnaona munavyoadhirika sasa?
ReplyDeletesasa kwanini anatolewa na askari? au jamaa walitaka kumchapa?
ReplyDelete