Habari za Punde

ZEPHE kurekebisha katiba yao

Na Kauthar Abdalla
KUNA umuhimu wa kutolewa elimu ya sheria za kazi kwa wafanyakazi na wanachama wa vyama vya wafanyakazi ili wajue mahitaji yao ya msingi.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Chama cha Huduma za Umma na Afya Zanzibar (ZUPHE) Abdalla Abdulhamid Haji, alipokuwa akifanya marekebisho ya katiba ya chama hicho katika ukumbi wa Eacrotanal mjini Unguja.

Alisema kwa kuwa taasisi hiyo imelenga zaidi kutoa huduma hivyo ipo haja kwa wanachama ambao ni wafanyakazi wa taasisi mbali mbali kujua sheria za kazi ili waweze kutetea maslahi yao kwa misingi inayotakiwa.

Aidha alisema katiba iliyokuwepo ya mwaka 2008 ina upungufu mwingi unaomnyima haki wanachama hivyo kuna haja ya kufanyiwa marekebisho.

Alisema lengo la kurekebisha katiba ya chama hicho ni moja ya hatua za kutatua migogoro kati ya muajiri na muajiriwa ili kupatikana haki na fursa stahiki pande zote mbili.


Nae Mjumbe wa chama hicho,Rehani Haji Suleimani, alisema katika marekebisho ya katiba hiyo ni vyema chama kifuatilie na kuhakikisha shughuli mbali mbali zilizolengwa zinatekelezwa.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.