STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 28.11.2014
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi mbali mbali katika
hafla iliyofanyika Ikulu mjini Zanzibar.
Viongozi walioapishwa
katika hafla hiyo ni Bwana Khamis Jabir Makame ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya
Kusini Unguja ambapo kabla ya uteuzi wake huo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya
Kaskazini ‘B’ Unguja, Luteni Kanali
Mstaafu Haji Makungu Mgongo ambaye ameapishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini ‘B’
Unguja ambapo kabla ya hapo alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kusini Unguja.
Bwana Hassan
Khatib Hassan ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Wete, Bibi Khadija Bakari Juma
ambaye ameapishwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Bibi
Madina Mjaka Mwinyi ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu (Taaluma) Wizara ya Elimu
na Mafunzo ya Amali.
Wengine ni Dk.
Said Seif Mzee ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Biashara, Viwanda na
Masoko, Dk. Juma Yakout Juma, ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya
Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo.
Hafla hiyo, ilihudhuriwa
na viongozi mbali mbali wakiwemo baadhi
ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar
Mhe. Said Hassan Said, Mkuu wa Mkoa wa
Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja
Meja Mstaafu Kasim Tindwa, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Naibu
Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali pamoja na Washauri wa Rais wa Zanzibar na viongozi wengine wa Serikali.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment