Habari za Punde

Michuano ya Wazi ya Mchezo wa Basketiball kwa Vijana U-17, Yakidhaminiwa na Hoteli ya Makungu ya Zanzibar Ocean View LI YA zANZIBAR oCEAN vIEW

 Kamati ya Maandalizi ya Michuano ya Wazi ya mchezo wa Kikapu kuibua vipaji kwa Vijana wadogo katika mchezo huo Zanzibar, Michuano hiyo imefadhiliwa na Mfanya Biashara ya Mahoteli Zanzibar Amani Ibrahim Makungu, ili kuinua mchezo wa Kikapu Zanzibar.
           Mchezaji wa Carvarious akibasketi mpira kujiandaa kumpita mchezaji wa New West.
Wachezaji wa New West wakipata maelekezo kutoka kwa kocha wao wakati wa kota ya pili ya mchezo huo uliofanyika viwanja vya maisara. 
Mchezaji mkongwe wa mchezo wa Kikapu Zanzibar Taso akitowa maelekezo kwa wachezaji wa timu yake wakati wa mapumziko ya mchezo huo.
             Mchezaji wa timu ya Kikapu ya New West akimpita mchezaji wa timu ya Cavarious.
Mchezaji wa timu ya Cavarious akiwa juu akipaga bao katika mchezo wao na New West uliofanyika uwanja wa maisara timu ya Cavarious imeshinda kwa vikapu 56-34

 Mchezaji wa timu ya Cavarious akipasketi mpira huku mchezaji wa Nwe West akimkimbilia katika mchezo huo.  
         Wapenzi wa mchezo wa Kikapu Zenj wakifuatilia mchezo huo katika viwanja vya maisara.
 Mchezaji wa timu ya New West akidanki juu kuingia basket katika mchezio huo uliofanyika viwanja vya maisara Zenj. 
 Mchezaji wa timu ya Cavarious , akijiandaa kumpita mchezaji wa timu ya New West katika mchezo wa kuibua vipaji kwa Watoto walioko chini ya U-17, michuano hiyo inafanyika katika viwanja vya maisara. 
Wapenzi wa mchezo wa mpira wa Kikapu Zanzibar wakifuatilia michuano ya Wazi kuinua Vipaji kwa Watoto walioko chini ya umri wa miaka 17, yaliofadhiliwa na Mfanyabiashara  maarufu  wa mahoteli ya Zanzibar Ocean View Zanzibar Ndg Ibrahim Makungu,yanafanyika katika viwanja vya maisara Zenj.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.