Na Joseph Ngilisho, Arusha
Wadau wa sekta ya utalii nchini
Ufaransa, wameisaidia Tanzania magari matano aina ya Toyota Land Cruiser yenye
thamani ya shilingi 599,338,330, yatakayotumika kupambana na ujangili katika
maeneo mbalimbali yenye uhifadhi wa wanyama pori nchini.
Msaada huo umekabidhiwa kwa Waziri
wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu na mwakilishi wa wadau hao hapa
nchini,Mohsin Shem,ambaye alieleza kuwa msaada huo umetokana na michango ya
taasisi mbalimbali za kusaidia na kupambana na ujangili nchini humo.
Alisema gari hizo zitasaidia kupunguza
changamoto inayotokana na ujangili,unaosababisha sekta ya utalii
kushuka,kupoteza watalii wa ndani na nje pamoja na kutoweka kwa wanyama ambao
ni kivutio kikubwa cha utalii nchini.
“Kwa umoja uliooneshwa na
taasisi za utalii,wameahidi kuendelea kutoa misaada mingine mingi ikiwemo
vitendea kazi vya kupambana na ujangili,lengo ni kuhakikisha wanatokomeza
vitendo vya uharamia wa wanyama nchini,” alisema.
Waziri Nyalandu aliwashukuru
wadau hao na kusema suala la ujangili nchini bado ni kubwa, hivyo alitoa wito
kwa wadau wengine kuendelea kujitokeza kupiga vita vitendo vya ujangili ili
kutokomeza kabisa.
Hata hivyo,alisema serikali ipo
mbioni kunununua helkopta mbili zitakazotumika kuongeza nguvu kwa kufanya doria
maeneo mbalimbali ya uhifadhi,huku helkopta iliyoanguka hivi karibuni ikiwa
mbioni kulipwa na bima.
Aidha alisema serikali
inakabiliwa na uhaba wa marubani,ambapo aliitaka jamii kujitokeza kusomea
urushaji wa ndege ili kupunguza changamoto hiyo,hata hivyo alizishukuru kampuni
mbalimbali za uwindaji zaidi ya 50 zilizojitokeza kumsomesha rubani wa
kike,Anna Lorayo (32) atakayesaidia kurusha ndege kwa ajili ya doria ya
kupambana na ujangili.
Hapa ndipo ninapoona kuwa katiba iliyopendekezwa haina maana sasa magari wamepewa Tanzania mbona sijaona pahala palipoainisha Zanzibar, au wamepewa Tanganyika?
ReplyDelete