Habari za Punde

Wateja wa Tigo na ZANTEL sasa kufurahia huduma salama na uhakika ya kutumiana fedha kwenye Mitandao yao kwa 100%

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Wateja wa Tigo na ZANTEL sasa kufurahia huduma salama na uhakika ya kutumiana fedha kwenye Mitandao yao kwa 100%
  
Zanzibar - 17 Desemba, 2014. Kampuni za simu za mkononi za Tigo na ZANTEL zamezindua rasmi huduma za kutumiana pesa miongoni mwa wateja wake Tanzania.  Mbali na huduma hiyo ya kutumiana pesa miongoni mwa wateja wa mitandao hiyo, wateja wa EzyPesa na TigoPesa sasa wataweza kutuma na kupokea pesa kwa marafiki na ndugu walio katika mitandao hiyo popote pale nchini.

Kutekelezwa kwa mpango huo kunazifanya Tigo na ZANTEL kuwa viongozi wa huduma kama hiyo Duniani.  Haya ni matokeo ya makubaliano yaliyotangazwa mwanzoni mwa mwaka huu na EzyPesa, TigoPesa na Airtel Money.  

Jinsi Huduma hiyo inavyofanya kazi:

Wateja wa Zantel:
Wateja wa Tigo:
1.      Piga *150*02#
1.      Piga *150*01#
2.      Chagua: Chaguo la 1 (Tuma Pesa)
2.      Chagua: Chaguo la 1 (Tuma Pesa)
3.      Chagua: Chaguo la 2 (Tuma TigoPesa)
3.      Chagua: Chaguo la 5 (Tuma EzyPesa)
3.1.   Ingiza Namba ya TigoPesa
3.1.   Ingiza Namba ya TigoPesa
3.2.   Ingiza Kiwango
3.2.   Ingiza Kiwango
3.3.   Ingiza Neno la Siri
3.3.   Ingiza Neno la Siri
3.4.   Subiri Uthibitisho wa Ujumbe Mfupi wa Maneno
3.4.   Subiri Uthibitisho wa Ujumbe Mfupi wa Maneno

Hakuna gharama za ziada mteja anapotuma pesa kwa mtandao mwingine isipokuwa gharama zinakuwa sawa na zile anapotuma kwenye mtandao wake.  Wateja wanaopokea pesa kutoka mtandao mwingine wanaweza kutoa pesa kwa wakala wa mtandao wao na hapatakuwa tena na ulazima wa mteja kutafuta wakala wa mtandao wa mtu aliyemtumia pesa.

Akizungumza kutoka Zanzibar, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Fedha wa Tigo, Andrew Hodgson alisema: “Tunafuraha kupanua wigo kwa wateja wetu kwa ubia na Zantel.  Hatua hii ni muhimu hasa kwa Zanzibar ambapo fursa ya kukua kwa huduma za fedha kwa mitandao ya simu bado ni kubwa.”

Anasema kama ilivyo kwa huduma nyingine za simu kama milio ya sauti na ujumbe mfupi wa maneno, kuna fursa kubwa ya kuimarisha huduma kwa wateja kwa kushirikiana badala ya kushindana baina ya wadau katika sekta ya mawasiliano kwa kupanua huduma za kutuma na kupokea fedha kwa kutumia mitandao Tanzania.
Anafafanua zaidi kuwa kwa kufanya kazi na wadau wengine, kunawawezesha kupanua wigo wa wateja na hivyo kwa pamoja kutoa huduma ambazo ni bora zaidi, salama, na za haraka kwa wateja wa pande zote.
“Ubia ambao tumeingia leo sio tu utaleta karibu kampuni zetu, bali muhimu zaidi ni ukaribu wa wateja wetu kwa kuwapatia huduma za fedha za kielektroniki bora zaidi ambazo hawakuweza kuzipata hapo awali,” alisema Hodgson. 
Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Mohamed Mussa, anasema Zantel inaendelea kutimiza ahadi ya kuwarahisishia huduma za fedha wateja wake kwa kufanya kazi pamoja na Tigopesa.

“Kwa kufanya hivi tunapanua wigo kwa wateja wetu, huduma hii inawawezesha zaidi wateja kutuma na kupokea fedha kwa urahisi zaidi,” anasema.

Anafafanua zaidi kuwa kwa huduma hii itasaidia kuimarisha huduma za fedha kati ya visiwa vya Zanzibar na Tanzania Bara.

“Zantel iko katika mstari wa mbele kuhakikisha kuwa ushiriki wa wananchi wa Zanzibar katika sekta muhimu ya fedha unaimarika na kukua.  Tumehakikisha kuwa mtandao wa mawakala wetu na watoa huduma wengine wako tayari kuwahudumia wateja wetu,” anasema Bw. Mussa.
 
About Zantel
Zantel currently serves a growing subscriber base and consistently demonstrates its core values of affordable, consistent and seamless services. Zantel believes that apart from offering a solid platform of technological innovation, sustainable investment is the bedrock of stellar growth and economic stability.We offers International Gateway services, Fixed, Mobile , data services through its CDMA, GSM , 3G networks and mobile Finance services popularly known as ‘Ezypesa”. 
Zantel is part of Etisalat Group which has been recognized as “Best Operator” 10 times since 2006 and “Best Wholesale Provider” 4 times in the last three years servicing 145 million customers in 15 countries. Etisalat continues to reach out to new customers and markets.
For further information about Zantel visit; www.zantel.co.tz
Arnold Madale – Senior Manager, Media and Brand
Mobile: 0779 222 344





About Tigo:

Tigo Tanzania is the leading innovative telecommunication company in the country, distinguished as a fully-fledged digital lifestyle brand. Offering a diverse product portfolio in voice, SMS, high-speed internet and mobile financial services, Tigo has pioneered innovations such as Facebook in Kiswahili, Tigo Pesa App for Android & iOS users, and East Africa’s first cross-border mobile money transfer with currency conversion. 

The Tigo 3G network guarantees the best services to its subscriber’s in all regions across the country.  Between 2013 and 2014 alone the company launched over 500 new network sites and plans to double its investment by 2017 in terms of coverage and additional capacity networks for deeper penetration in rural areas. With over seven (7) million registered subscribers to their network, Tigo directly and indirectly employs over 100,000 Tanzanians including an extended network of customer service representatives, mobile money merchants, sales agents and distributors.

Tigo is the biggest commercial brand of Millicom, an international company developing the digital lifestyle in 44 countries with commercial operations in Africa and Latin America and corporate offices in Europe and the USA. With the certain knowledge that only constant innovation will keep them on top, Millicom keeps creating greater shareholder value; applying their concept of “demand more” is how they do business and retain their position as digital lifestyle leaders in some of the most unique and challenging markets.

“SMILE, YOU’RE WITH TIGO”

For further information about Tigo visit:  www.tigo.co.tz  Or contact:
John Wanyancha – Corporate Communications Manager
Mobile: 0658 123 089





No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.