Hifadhi hiyo imejumuisha vijiji tisa vikiwemo Pete , Kitogani ,Ukongoroni chwaka ,Charawe ,Unguja ukuu, Michamvi na
Cheju .
Taratibu tunaingia
katika hifadhi ya
msitu huo ghafla
tunaona kuna vitu
vya aina mbali mbali vya ajabu ambayo ni vivutio vikubwa vya utalii ambao huwavutia watu kutoka kila
kona ya Dunia.
Vivutio hivyo
vimegawika katika sehemu tatu vikiwemo daraja la mikoko,sehemu Kima punju na
Msitu.
“Msitu huo una
miti ya aina mbali mbali kama mitondoo, mivinje ,
mikaratusi miti mafuta, mikonge, mikangara shamba na mingi mingineyo, ambayo
ina urefu wa ajabu na kushonana juu yake jambo ambalo hufanya jua lisionekane
katika eneo hilo,”Alisema ndugu Ali Khamis Moh”d ambae ni mkuu wa hifadhi ya msitu wa
Jozani,alipoanza simulizi juu ya hifadhi hiyo.
Alisema kuna
baadhi ya miti ni dawa na hii mara nyingi hupatikana katika msitu huu wa Jozani
kama vile Misiliza ambayo hutumika kama
dawa ya kuondoa minyoo tumboni.
“Na baadhi ya miti mingine hutumika katika
kutengenezea mafuta mfano mti wa mkunazi,”aliongeza mkuu wa Hifadhi hiyo.
Pia alisema katika msitu wa hifadhi wa Jozani kuna wanyama
adimu ambao hawapatikani katika hifadhi nyengine yoyote kwa mfano chura wa Jozani,Chuwi wa Zanzibar,Jongoo wa
Jozani,Kima Punju,Paa nunga na wingineo
wingi.
“ Hata hivyo katika Wanyama wote hao Kimapunju ndio
kivutio kikuu cha watalii kutokana na rangi yake ,umbile na tabia yao ya kuishi
ujamaa kama Binaadamu,”alieleza ndugu Ali.
Alizungumzia
kidogo juu ya Kima punju alisema huishi na kufuatana kwa makundi na kila kundi
huwa mna dume mmoja na kamwe hakubali kuliacha kundi hilo kuingiliwa na dume
mwengine hadi kufa kwake.
Vile vile
alisema Kima punju hupendelea sana kula majani
machanga ya miti kama vilele vya mipera na majani ya mikungu ambayo ndio
hupendelea kula zaidi jambo ambalo husababisha mikungu yote ya Jozani kutokuwa
na majani kabisa kwani yakichipua tu
huliwa.
Alisema wanyama
hao hula maganda ya matunda kama vile
Embe,Mapera na makoroma ya nazi na hawali kabisa matunda yenye sukari kama vile Embe mbivu ,Ndizi mbivu kutokana na matumbo yao kushindwa kusaga vitu
vya sukari(insuline hormone).
“ Kima punju hula makaa meusi kama ni tiba ya maradhi mbali mbali
yanayowasumbua na ni kinga ya maradhi
yao,” alifahamisha.
“ Vile vile Kima
punju hukaa zaidi ya miezi mitano bila
ya kunywa maji kutokana na vyakula wanavyokula si vya kunywesha maji, kwani
mara nyingi hula vyakula vyenye ukafu vikiwemo vilele vya majani machanga,” alifafanua ndugu Ali.
Licha ya kuwa
Kima punju kuwa ni kivutio kikuu cha
watalii pia Chura wa Jozani anaepatikana katika Bwawa la maji baridi la
Mwanjoza nae ni kivutio kikubwa kutokana na kuwa ni mnyama pekee anaepatikana
Jozani tu .
“ Pia aliendelea
kwa kusema kila baada ya miaka kumi na
tano (15) huvumbua mnyama au mti mpya katika hifadhi hiyo, kwa miaka kumi na tano (
15) iliyopita tulivumbua Chura wa Jozani katika Bwawa la Mwanjoza”,alisema mkuu
huyo wa Hifadhi.
Alisema Bwawa la Mwanjoza ni Bwawa la ajabu lililopo
katikati ya msitu wa Jozani, kutokana na kuwa na vitu vya ajabu kama miti
iliyoota chini ya maji na mizizi yake
kutokeza juu ya Bwawa,Miti iliyoota juu ya miti mwenzao na mengine iliyoota juu ya maji kama mayungi
yungi yenye maua ya kupendeza .
“ Kwa kweli
Bwawa la Mwajoza linaongeza hadhi ya uzuri wa msitu wa hifadhi wa Jozani kwani licha miti hiyo pia kuna chura wa
Jozani alivumbuliwa katika Bwawa hilo,”aliongeza.
Baada ya
kuondoka katika Bwawa la Mwajoza tulielekea katika Daraja la Mikoko ambapo
tulichukuwa dakika 40 kutembea kwa miguu .
Njiani tuliona
vipepeo aina mbali mbali kama Dadanesi nawengine wengi wenye rangi ya kupendeza
kama Karasisi ambae hupatikana Zanzibar
tu.
Tukiwa
tunaendelea na safari ghafla tuliona Bango la mradi wa Kasa tulipouliza alisema
kuwa “huo ni mradi wa Tassaf na hausiani
kabisa na hifadhi ya Msitu wa Jozani,”alifafanua ndugu Ali.
Baada ya
dakika kumi tulifanikiwa kufika katika
Daraja la Mikoko ambapo huko kuliwa na uzuri wa ajabu kutokana na Miti
hiyo ya Mikoko kushonana na kunawiri vizuri katika maji chumvi yalioko chini ya
Daraja hilo la mbao.
Mikoko hiyo
ipo ya aina tatu : mikoko meupe,mikoko meusi na mikoko mekundu(magando) ambayo ndio inaengeza
hadhi ya Daraja hilo kutokana na miti hiyo kuwa na matawi mengi na mizizi yake
huchomo juu ya ardhi kwa kiasi kikubwa jambao ambalo huwezi kuwamini kama
mizizi waweza hisi nayo ni jumla ya matawi ya miti hiyo.
Nae Mkuu wa kitengo
cha Utalii ndugu Salum Ramadhani alisema kuwa Msitu wa Jozani ni miongoni mwa sekta
muhimu ya utalii yenye kuingiza fedha nyingi kwa serikali,kutokana na kuwa na vivutio vya
kila namna katika hifadhi hiyo.
“ Kila mwaka tunapokea wageni kutoka
sehemu mbali mbali ndani na nje ya nchi takribani 25,000 kwa mwaka ambao huchangia zaidi ya Tsh milioni 400,” alifafanua ndugu
Salum Ramadhani.
“ Aidha
alisema wageni wengi
kutoka nchi za Ujerumani,
Uingereza, Marekani,Ufaransa na Italia, Wageni wengi zaidi hutoka utaliana kutokana na kuwa na usafiri wa moja kwa moja,” aliendelea
kueleza ndugu Salum.
Aliendelea kwa
kusema kuwa mapato yanayopatikana
kutokana na uingiaji wa wagani hao hugawiwa katika mafungu mawili alifahamisha kuwa,Fungu
la kwanza ni la serikali ambalo ni asilimia 50 na fungu la pili ni la wanavijiji
ambalo nalo ni asilimia 50 kwa wanavijiji waliozunguuka hifadhi hiyo.
“ Hii
ni Kutokana na kuharibiwa mazao yao
na wanyama waharibifu kama kima,Nguruwe pamoja na wanyama wengine na
kukosa maeneo ya kutosha kwa ajili ya kilimo kikiwemo kijiji cha Pete kutokana na eneo
kubwa la ardhi yao kuingia ndani ya
hifadhi hiyo,” alifafanua ndugu Salum.1/29/2015
Nae mmoja miongoni mwa wanavijiji hao ndugu Moh’d Ali
Mchobwa alisema kuwa kwa sasa wanafaidika
na hifadhi hiyo kwa kupokea fedha
kutoka katika mgao wa kila mwaka na
kufanikiwa kujenga skuli kwa maendeleo ya watoto wao.
“Zamani walikuwa watoto wanapata tabu sana
maana wanatembea masafa marefu kufuata Elimu kwenye vijiji vya mbali kama vile
Kitogani na Muyuni” .alisema ndugu Mchobwa.
Hata hivyo ,mkuu
wa hifadhi hiyo alisema, licha ya Hifadhi hiyo kuwa na faida nyingi pia
hukabilwa na changamoto mbali mbali zikiwemo kuungua moto kila baada ya mwaka kutokana na mkusanyiko wa majani mengi ambayo
hupelekea kuwaka moto wenyewe.
Aidha sababu
nyengine zinazopelekea msitu huo kuungua moto ni uvunaji haramu wa Asali pamoja na wasasi
ambao hutafuta wanyama kama nguruwe na Paa kwa ajili ya kitoweo,Hivyo kutokana na kazi hiyo ngumu ya uwindaji
ambayo hufanywa wakati wa usiku baadhi
ya wasasi huvuta sigara na vipande hutupwa na kusababisha mlipuko wa moto.
Pia aliendelea kwa kusema kuwa wanao walinzi mbali mbali lakini bado suala hilo
linakuwa guumu kutokana na ukubwa wa
Hifadhi hiyo.
Alisema kutokea kwa moto husababisha kukimbia kwa wanyama kama vile paa na hata wanyama wengine ambao ni wazito
kukimbia hufa mfano Chatu, Nyoka na hata
wadudu wadogo wadogo wakiwemo Jongoo wa Jozani pamoja na miti ya asili
kutoweka.
Hifadhi ya
Jozani si hifadhi ya kuoteshwa bali ya asili
na rasilimali zilizomo zimehifadhiwa
tangu zamani.
Katika eneo la Jozani palikuwa na mtawala
aliyejulikana kwa jina la JOSHI, ambae alikuwa mfanya biashara wa
kihindi.Mfanya biashara huyo alikuw
a akiishi eneo hilo mnamo mwaka 1930 hadi kufikia 1996 msitu huu
ulirejeshwa mikononi mwa wanavijiji ilikuwa ni hatua ya kwanza kuhifadhi na
kuulinda.
Mfanya biashara
huyo ambae alikuwa akiishi karibu na Bwawa la Mwajoza ambalo
alikuwa akitumia kwa shughuli mbali
mbali za kila siku, Hivyo jina la mtawala Joshi na eneo alilokuwa akiishi Mwajoza ikapelekea
kupatikana kwa jina la Jozani.
No comments:
Post a Comment