Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad akitembelea wodi mpya ya wagonjwa mahututi (ICU), katika hospitali ya Mnazi Mmoja, baada ya kuifungua rasmi.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha afya Mbweni, wakiwa sehemu ya washiriki katika hafla ya ufunguzi wa wodi ya wagonjwa mahututi katika hospitali ya Mnazi mmoja.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akisisitiza jambo wakati wa ufunguzi wa kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU), katika hospitali ya Mnazi Mmoja.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dr. Mohamed Saleh Jidawi, akizungumza wakati wa ufunguzi wa kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU), katika hospitali ya Mnazi Mmoja.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akigana na Balozi mdogo wa China aliyepo Zanzibar Bw. Xie Yun Liang, baada ya kumalizika hafla ya ufunguzi wa kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU), katika hospitali ya Mnazi Mmoja. Wa pili kulia ni Waziri wa Afya Mhe. Rashid Seif Suleiman. (Picha na Salmin Said, OMKR)
No comments:
Post a Comment