Habari za Punde

Mama Asha Akabidhi Tanuri la Kuchomea Taka Kituo cha Afya Kitope.

Mama Asha Suleima akizungumza na baadhi ya watendaji wa Kituo cha Afya cha Kitope mara baada ya kukabidhi Tanuri la kuhifadhia taka taka zinazokusanywa ndani ya Kituo hicho.
Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi akimkabidhi Tanuri la kuhifadhia taka taka Mkuu wa Kituo cha Afya Cha Kitope Dr. Ameir Yunus  Makame.
Tanuri la kuhifadhi taka taka zinazozalishwa katika Kituo cha Afya cha Kitope lililojengwa na kugharamiwa na Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali ili na kuungwa Mkono na Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “ B”.

Na Othman Khamis Ame                                                                                      
Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi amewakumbusha Wafanyabiashara na Wananchi kuendelea kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa wakati ili fedha zinazokusanywa na Halmashauri za Wilaya zao ziweze kuongeza nguvu katika kusaidia kuiendeleza miradi yao ya maendeleo.

Alisema nguvu za baadhi ya Halmashauri hapa Nchini zinakuwa ndogo kuunga mkono miradi ya Wananchi kutokana na baadhi ya wananchi hasa wafanyabiashara kukweka kulipa kodi kitendo ambacho pia kinakosesha mapato Serikali Kuu.


Mama Asha Suleiman Iddi alitoa kumbusho hilo wakati akikabidhi tanuri la kuchomea taka taka { Placentar Pits } katika Kituo cha Afya cha Kitope Kiliomo ndani ya Jimbo la Kitope Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Ujenzi wa Tanuri hilo uliogharamiwa na Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi na kuungwa mkono wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini “ B “ulifuatia ziara aliyoifanya Kituoni hapo Tarehe 3 Machi Mwaka 2013 na kuelezwa changamoto zinazokikabili Kituo hicho.

Mama Asha alisema uwepo wa Tanuri hilo ambalo ilikuwa kilio cha muda mrefu kwa wafanyakazi wa Kituo hicho umelenga kuhifadhi mabaki ya taka taka zinazozalishwa kituoni hapo ambazo kuachiwa kwake zingeweza kusababisha maambukizo ya maradhi mbali mbali.

Alimpongeza Mbunge wa Jimbo la Kitope ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kwa juhudi anazoendelea kuchukuwa katika kusaidia kuunga mkono miradi inayoanzishwa na Wananchi  ndani ya Jimbo hilo.

Aliwatahadharisha Wananchi wa Jimbo hilo kujiepusha na choko choko zinazoendelea kupenyezwa na baadhi ya watu ndani ya Jimbo hilo zikielezkezwa zaidi kwa vijana kwani kuachiwa kwake zinaweza kuviza maendeleo yaliyopatikana Jimboni humo.

Akitoa shukrani Mkuu wa Kituo hicho Dr. Ameir Yunus alisema changamoto ya ukosefu wa Tanuri hilo ilikuwa ikiwapa wakati mgumu wafanyakazi wa kituo hicho katika kukabiliana na taka taka zilizokuwa zikikusanywa ndani ya Kituo hicho.

Dr. Yunus alisema changamoto ya ukosefu wa Tanuri hilo ilikuwa ikiwapa wakati mgumu wafanyakazi wa Kituo hicho katika kukabiliana na taka taka zilizokuwa zikikusanywa ndani ya Kituo hicho.

Mkuu huyo wa Kituo cha Afya cha Kitope aliwaomba akina mama waja wazito wa Jimbo hilo na vitongoji vyake kukitumia kituo hicho katika kupata huduma za afya pamoja na zile za waja wazito ili wawe na uhakika wa kujifungua salama.

Dr. Yunus alifahamisha kwamba ule wakati wa akina mama kwenda kituoni hapo na Majembe kwa ajili ya kupata huduma za uzazi umekwisha kabisa baada ya kupatikana kwa Tanuri hilo.

Tarehe 3 Machi Mwaka 2013 Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi alifanya ziara ya kukikagua Kituo cha Afya cha Kitope na kutoridhika na mazingira aliyoyakuta ya Kituo hicho.

Aliwakumbusha wafanyakazi wa Kituo hicho kuzingatia usafi wa mazingira yanayokizunguuka kituo hicho ili kuepuka maradhi yanayoweza kuwakumba wagonjwa wanaofika kituoni hapo ambapo aliahidi kuwajengea Tanuri la kuhifadhia taka taka.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.