Habari za Punde

JK aagiza kutengwa maeneo ya uwekezaj

Na Kija Elias, Moshi
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dk Jakaya Mrisho Kikwete, ameagiza  uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro chini ya mkuu wake wa mkoa, Leonidas Gama, kutenga maeneo ya kutosha kwa ajili ya uwekezaji ikiwamo viwanda vitakavyowezesha  kuwe`po vitega uchumi vingi katika mkoa  huo.
Alitoa ushauri huo mkoani Kilimanjaro katika hafla ya uzinduzi wa  jengo  la kisasa la kitega uchuni ambalo limejengwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii,NSSF, na kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 64 hadi kukamilika kwake.
Alisema nchi yeyote duniani haiwezi kupiga hatua kimaendeleo na kiuchumi bila viongozi kukaa pamoja kuweka mazingira ambayo yatasaidia kuinua uchumi wa mkoa huo na maeneo husika.

Aliwataka viongozi hao kutengeneza mazingira wezeshi katika kutenga maeneo ya uwekezaji yatakayokuwa rafiki kwa wawekezaji ambao watakuwa tayari kuwekeza katika mkoa huo tofauti na sasa ambako wawekezaji wengi wamekuwa wakikimbilia katika mkoa jirani wa Arusha.
Alisema uwepo kwa jengo hilo la kisasa ambalo limekuwa kivutio kikibwa katika mji wa Moshi unaotarajiwa kuwa jijiji hivi karibuni,kutawavutia watu wengi kuendesha shughuli zao za kibiashara pamoja na mikutano ya kimataifa.
Katika hatua nyingine,Rais Kikwete aliwataka wanasiasa kuacha kutumia ubabe kwa kupinga shughuli za maendeleo  ambazo zimekuwa zikitekelezwa na mkoa huku akimlenga Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi,Jaffari Michael.
Alimtaka Meya huyo kuwa mstari wa mbele kuunga mkono shughuli za maendeleo badala ya kuwa mpinga maendeleo namba moja na kuacha mbwembwe za kisiasa ambazo haziwezi kuleta maendeleo kwa wakazi mji wa Moshi. 
Awali akimkaribisha Rais Kikwete, Mkuu wa mkoa huo, Leonidas Gama, alisema uwepo wa jengo hilo utachangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumia wa mkoa, na kwamba watilii wanaofika na kutembelea mlima Kilimanjaro watafika katika jengo hilo na kujipatia mahitaji yao kabla ya kupanda mlima huo.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa hiyo, Jaffari Michael, alisema tayari halmashauri hiyo imekwisha kutenga maeneo ambayo yatatumika kama vitega uchumi vya mkoa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.