TUME YA UCHAGUZI YA
ZANZIBAR
Taarifa ya Mwenyekiti
wa Tume ya Uchaguzi Mhe. Jecha Salim Jecha Katika
Mkutano na Waandishi wa
Habari Juu ya Mabadiliko ya Idadi, Mipaka na
Majina ya Majimbo ya
Uchaguzi ya Zanzibar
Tarehe 6 Julai, 2015
Hoteli ya Grand Palace
Malindi
Wawakilishi wa Vyombo
vya Habari;
Viongozi wa Asasi za
Kijamii;
Mabibi na Mabwana.
Assalam Aleykum
Kwanza kabisa naomba nichukuwe nafasi hii kumshukuru
Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana tukiwa wazima na wenye afya. Kwa niaba
ya Tume ya Uchaguzi natoa shukurani nyingi kwa kukusanyika nasi muda huu ili
kusikiliza taarifa muhimu tutakayoiwasilisha kwa wananchi na wadau wa uchaguzi kupitia
katika vyombo mbalimbali mnavyoviwakilisha.
Katika mkusanyiko wa leo tutaitoa taarifa hiyo, lakini
naomba muwe na subira kidogo na msikilize maelezo mafupi juu ya chanzo cha kazi hii na
katika kuifanya kazi hii ni mambo gani muhimu yaliyozingatiwa na Tume
Ndugu Waandishi,
Katiba ya Zanzibar, 1984, Kifungu cha 120(4), kinaielekeza, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuwa katika kipindi cha miaka 8 hadi
10 au wakati mwengine wowote, kuchunguza idadi ya mipaka na majimbo ya uchaguzi na
baada ya uchunguzi
wake inaweza kubadili idadi, mipaka na majina ya majimbo
hayo.
Ndugu Waandishi,
kwa kuzingatia maelekezo hayo ya kisheria na kwa kuwa ilikuwa tayari inakaribia miaka 10 tangu mapitio ya mwisho ya
majimbo ya uchaguzi yalipofanyika (2004), na kwa kuwa kuacha kuitekeleza kazi
hizo, Tume ingekuwa inakiuka Katiba ya Zanzibar, Juni 2014 Tume iliandaa
Mpangokazi wa kazi ya uchunguzi wa majimbo na iliusambaza mpango kazi huo kwa
Wadau mbalimbali vikiwemo vyama vya siasa.
Mpangokazi huo ulikuwa na maeneo manane ambayo yalipangwa
kutekelezwa na Tume katika kazi hiyo. Maeneo hayo ni utoaji wa taarifa kwa
wadau juu ya kazi ya uchunguzi wa majimbo na kupitia vyombo vya habari na
mikutano na wadau tuliwajulisha wananchi juu ya kazi hiyo muhimu.
Eneo jengine lilikuwa ni kupokea maoni ya vyama vya siasa.
Katika kazi hii, Tumeilikutana ana kwa ana na Wawakilishi wa vyama 18 vya siasa
vyama vinne vilituma maoni yao kwa maandishi.
Aidha, Tume ilipokea maoni kutoka
Taasisi za Serikali ambapo katika utaratibu huu tulikutana na Wakuu wa Mikoa na
Wakuu wa Wilaya,tulikutana na Wawakilishi wa Wizara zote zinazohusika na
masuala ya Utawala Bora,masuala ya Tawala za Mikoa, Jeshi la Polisi. Vile vile,
tulikutana na Viongozi wa kuchaguliwa kama vile vile Wawakilishi, Wabunge na Madiwani
wote wa Unguja na Pemba na hatimae tulifanya mikutano ya wazi ya upokeaji wa
maoni ya wananchi na Asasi za kijamii kwa Wilaya zote.
Ndugu Waandishi,
baada ya mikutano yote hiyo na wadau tulifanya ziara za kutembelea maeneo ya mipaka ya Shehia yaliyolalamikiwa
wakati wa kupokea maoni pamoja na kuwa maeneo hayo yako chini ya mamlaka nyengine,
tulitembelea mipaka ya wadi na majimbo yote yaliyokuwa yanagusiwa sana wakati wa
kupokea maoni.
Tume ililazimika kutembelea maeneo yote yaliyolalamikiwa
nchi nzima, ili kuona maeneo ya mipaka ya majimbo na wadi yaliyolalamikiwa wakati
wa upokeaji wa maoni na hatimae kufanya uchambuzi wa maoni yote.
Uchambuzi wa maoni yaliyopokelewa ulifanyika kwa kuzingatia
maelekezo ya Katiba, Kifungu cha 120(3) kinasomeka kuwa ; majimbo yote yatakuwa
karibuni na wakaazi sawasawa kama inavyoonekana na Tume, lakini Tume inaweza kuepuka shuruti hii
kwa kiwango kile kinachofikiria kuwa inafaa kwa ajili ya
kuzingatia
i. idadi ya watu na zaidi katika kuhakikisha
uwakilishi unaofaa katika miji mikubwa na miji ya mashamba yenye idadi ndogo ya watu;
ii. ukuaji wa idadi ya watu;
iii. njia za usafiri; na
iv. mipaka ya sehemu ya utawala.
Ndugu Waandishi
kutokana na maoni ya wadau, ziara ambazo tulizifanya katika maeneo mbalimbali na takwimu zinazohusiana na watu na
makaazi, Tume ilishawishika kuwa kuna ongezeko kubwa la idadi ya watu katika baadhi ya
majimbo na eneo lililozidiwa sana ni Wilaya ya Magharibi.
Eneo hilo limeonyesha kuwa na ongezeko kubwa la idadi ya
watu kulinganisha na eneo jengine lolote lile la Zanzibar. Lakini kwa kutumia vigezo
hivyo hivyo, Tume ilibaini kuwa kuna baadhi ya majimbo ambayo yana idadi ndogo sana ya
watu.
Kufuatia matokeo hayo ya uchunguzi, Tume ilikubaliana kuwa
kuna haja kubwa ya kufanya marekebisho ya idadi, majina na mipaka ya majimbo ya
uchaguzi kwa kuzingatia maelekezo ya Sheria yanayoelekeza kuwepo na
uwiano wa watu baina ya jimbo na jimbo.
Ndugu Waandishi,
Tume tayari imekamilisha taarifa ya kazi ya uchunguzi wa idadi, majina na mipaka ya majimbo na iko tayari kuitangaza rasmi
mipaka mipya ya majimbo ya uchaguzi kwa umma. Kazi hii kwa asilimia mia
kubwa sana imefanywa kwa
kuzingatia maoni ya wadau wote. Tume ya Uchaguzi imeongeza
idadi ya majimbo ya Uchaguzi na hivyo kupelekea mabadiliko makubwa ya mipaka ya
majimbo kwa takriban majimbo yote. Mabadiliko hayo yatapelekea baadhi ya
majina ya majimbo
kubadilika.
Ndugu Waandishi
Tume ya Uchaguzi inapenda kutoa taarifa kuwa imekamilisha kazi yake ya uchunguzi wa Idadi, Mipaka na Majina ya majimbo ya
Uchaguzi. Tume imeongeza idadi ya majimbo manne ya uchaguzi ya Wawakilishi
na kufanya jumla majimbo yote kuwa 54 badala ya 50 yalokuwa ya awali. Baada
ya maelezo hayo, sasa naomba niwatangazie majimbo ya uchaguzi yatakayotumika
katika uchaguzi wa mwaka 2015.
No comments:
Post a Comment