Habari za Punde

Rais Dk. Shein, Afutarisha Wananchi wa Kijiji cha Mkanyageni Pemba jana

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Pemba                                                                                                           3.7.2015
---
WANANCHI wa Mkanyageni, Mkoa wa Kusini Pemba wamepongeza juhudi kubwa zilizochukuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein za kuhakikisha amani, utulivu na mshikamano miongoni mwa wananchi vinaimarika kwa lengo la kuleta maendeleo.

Hafla hiyo ya futari ilifanyika katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni, na kuhudhuriwa na wananchi wa kijiji hicho na vijiji vya jirani pamoja na viongozi mbali mbali wa Mkoa huo pamoja na baadhi ya viongozi wa Serikali.

Aidha, Mama Mwanamwema Shein naye aliungana pamoja na akina mama wenzake wa kijiji hicho cha Mkanyageni katika futari hiyo ya pamoja.

Wananchi hao waliyasema hayo wakati wakitoa neno la shukurani katika futari maalum walioandaliwa na Alhaj Dk. Shein hapo kijijini kwao Mkanyageni ikiwa ni  utamaduni aliouweka wa kufutari nao pamoja kila ufikapo mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Akitoa neno hilo la shukurani kwa niaba ya wananchi wa Mkanyageni, Maalim Abdalla Yussuf alisema kuwa katika uongozi wa Alhaj Dk. Shein wananchi wameshuhudia mshikamano mkubwa sambamba na kuwepo kwa amani na utulivu ambavyo ndio dira ya maendeleo.

Maalim Abdalla alisema kuwa mbali ya shukurani kwa futari hiyo aliyowaandalia pia, wananchi wa Mkanyageni wanatoa shukurani za pekee kwa Alhaj Dk. Shein kwa kuifanyia mema Zanzibar.

Mara baada ya futari hiyo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, Mkuu wa Wilaya ya Mkoani, Hemed Suleiman Abdalla alitoa shukurani kwa wananchi wote waliohudhuria katika hafla hiyo.

Alhaj Dk. Shein alieleza haja ya kuendeleza ushirikiano na mshikamano uliopo miongoni mwa wananchi wa Zanzibar sambamba na kuendelea kuishi kwa amani na utulivu.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Mkoani  Mkoa wa Kusini Pemba Bw.Hemed Suleiman wakati alipowasili katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni katika futari iliyoitayarisha kwa Wananchi wa Kijiji cha Mkanyageni  Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini  Pemba
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba Bi Hanuna Ibrahim Masoud wakati alipowasili katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni katika futari iliyoitayarisha kwa Wananchi wa Kijiji cha Mkanyageni  Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini  Pemba 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akishiriki katika swala ya magharibi iliyoswalishwa na Sheikh Chumu Salim  kabla ya futari iliyoitayarisha kwa Wananchi wa Kijiji cha Mkanyageni  Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini  Pemba jana  katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni
Akinamama wa Vijiji tofauti vya  Mkoa wa Kusini Pemba wakiwa katika futari iliyotayarishwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein jana  katika viwanja vya Skuli ya Mkanyageni
Wananchi na Waislamu wa  Kijiji cha  Mkanyageni Wilaya ya Mkoani  Mkoa wa Kusini  Pemba wakiwa katika  futari iliyotayarishwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein jana katikaviwanja vya Skuli ya Mkanyageni
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) Viongozi wengine wakiitikia dua iliyoombwa baada ya kufutari pamoja na Wananchi wa Kijiji cha  Mkanyageni Wilaya ya Mkoani  Mkoa wa Kusini  Pemba jana katika viwanja vya Skuli ya Mkanyagen
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein kushoto) akiagana na Wananchi wa Kijiji cha  Mkanyageni Wilaya ya Mkoani  Mkoa wa Kusini Pemba baada ya futari ya pamoja aliyoitayarisha kwa Wananchi wa kijiji hicho jana

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.