Habari za Punde

Wahariri wa Vyombo Mbalimbali vya Habari Wafurahia Ziara katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Saanane

Baadhi ya Wahariri na Waandishi wa habari wakiwa katika Boti maalumu kwa ajili ya safafri ya kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Saanane jijini Mwanza.

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa ,TANAPA,Pascal Shelutete alikuwa ni miongoni mwa wahifadhi walioongoza kundi hilo la Wahariri na Wanahabari kuelekea hifadhi ya Saanane.
Baada ya safafri ya takribani dakika 10 hatimaye Wahariri na Wanahabari wakawasili hifadhi ya Taifa ya Saaanane.
Safari ya kutembelea maeneo mbalimbali katika hifadhi hiyo ilianza.
Wahariri walipata maelezo katika maeneo tofauti tofauti.
Wakati mwingine katika mapitio ndani ya Hifadhi hiyo,wahariri na wanahabari walilazimika kupita kwa staili ya kutambaa.
Wengine walihitaji pia msaada ili waweze kuvuka kwa baadhi ya  maeneo .
Baada ya safari ya muda mrefu ,ndipo wakafika katika jiwe la kuruka na kuamua kupumzika.
Mazoezi ya kuruka yakaanza sasa.
Mhariri wa Channel ten Esther Zeramula akionesha umahiri katika kuruka katika eneo hilo.
Mhariri Jackton Manyerere pia hakua nyuma kuonesha umahiri wake.
Mhariri Mniku Mbani pia .
Wengine tukapata picha ya pamoja kwa ajili ya kumbukumbu.
Safari ya kurudi ikaanza kwa kundi la kwanza la Wahariri..
Wakati huo kundi la pili ndio lilikuwa likiwasili katika eneo hilo.
Baada ya kufika taswiraz zikaanza kuchukuliwa ,kama inavyoonekana hapa mhariri Dulinga akimchukua taswira mhariri Theofily Makunga.
Pozi za picha nazo hazikuwa mbali kwa baadhi ya wahariri.
Picha zaidi muelekeo wa ziwani.
Wahariri wakaoneshana umahiri katika kuruka .
Kama iliyokuwa kwa kundi la kwanza hawa nao wakapata picha ya pamoja.
Kisha safari ya kurudi ikaanza  huku wakifurahia Mandhari ya ziwa Victoria.

Na Dixon Busagaga wa Globuya Jamii Kanda ya Kaskazinia aliyeko jijini Mwanza.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.