Mkurugenzi Mkuu wa
Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa
akielezea machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi wakati wa Kikao cha
Pili cha Baraza la Nne la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo lililofanyika jana katika
ukumbi wa Hazina Ndogo mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Selina Kombani akiwahutubia wajumbe
waliohudhuria Kikao cha Pili cha Baraza la Nne la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa
ya Takwimu lililofanyika jana katika ukumbi wa Hazina Ndogo mkoani Dodoma.
Mkurugenzi
Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa (Kulia) akipiga makofi mara
baada ya Mgeni rasmi kufungua Kikao cha Pili cha Baraza la Nne la Wafanyakazi
wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu lililofanyika jana katika ukumbi wa Hazina Ndogo mkoani
Dodoma. Kushoto kwake ni Katibu wa Baraza hilo Magreth Jacob.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Selina Kombani akimkabidhi
cheti Mfanyakazi bora wa mwaka 2014 Joshua Mwaisemba mara baada ya kufungua Kikao
cha Pili cha Baraza la Nne la Wafanyakazi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu
lililofanyika jana katika ukumbi wa Hazina Ndogo mkoani Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Selina Kombani akimkabidhi
hundi mmoja wa wastaafu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Ibrahimu Masanja mara
baada ya kufungua Kikao cha Pili cha Baraza la Nne la Wafanyakazi
wa Ofisi hiyo lililofanyika jana katika ukumbi wa Hazina Ndogo mkoani Dodoma
Mgeni rasmi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Selina Kombani (wa tatu
kutoka kushoto) akiwa na wajumbe wa Baraza la nne la wafanyakazi wa Ofisi
ya Taifa ya Takwimu
mara baada ya kufungua Kikao cha Pili cha Baraza hilo kilichofanyika
jana katika ukumbi wa Hazina Ndogo mkoani Dodoma. (PICHA ZOTE NA VERONICA
KAZIMOTO - DODOMA).
No comments:
Post a Comment