Habari za Punde

Uhamiaji haramu washamiri Chwaka

     Na Miza Othman, Maelezo

Uhamiaji haramu umeshamiri katika kijiji cha  Chwaka, wilaya ya kati Unguja, na kupelekea ongezeka  la vitendo vya uhalifu katika shehia hiyo .

Sheha wa shehia ya Chwaka Simai Msaraka Pinja ameleeza hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea kijiji hicho.

Amesema katika  siku za karibuni  kumejitokeza  wimbi kubwa la kuingia wageni hasa  wakati wa usiku na kuondoka majira ya alfajiri bila kujua malengo yao na  wamejenga dhana kuwa watu hao wanaingiza madawa ya kulevya.

Sheha  Simai  amesema uongozi wa Shehia  kwa kushirikiana na jeshi la  polisi na askari jamii   wameaanzisha uchunguzi wa kujua maeneo wanayofikia watu hao na wenyeji wao ili kuweza kuwadhibiti..


Amesema  baadhi ya vijana  wa Shehia  ya chwaka   wamekuwa wakishirikiana na wageni hao  na tayari kumejitokeza dalili za vitendo viovu na baadhi wameanza kuathirika na dawa za kulevya..

Aidha alisema  ongezeko la watu katika shehiya yake ni jambo linampelekea kutojuwa takwimu  za uhakika na kupelekea  kukosa mahitaji ya lazima  ya  wananchi katika shehiya yake.


Aliwataka  wananchi kuwa makini katika kijiji chao na  wakiona  watu  wasio wafahamu  wapeleke taarifa kwa sheha ili kudhibiti wimbi kubwa la ongezeko la wahamiaji haramu .                                                                                 

Alitowa wito kwa vijana  waachane na vikundi viovu  na wajishuhulishe   kufanya kazi wakizingatia kuwa vijana ndio nguvu ya taifa   katika nchi.


Aliomba Serikali  iweke vidhibiti katika bandari  ndogo ndogo ili  wanaoingia  na kutoka waweze kujulikana  na watakaovunja sheria za nchi  waweze kushukghulikiwa na vyombo vya sheria.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.