Habari za Punde

Christopher Mtikila afariki dunia kwa ajali ya gari

Mwanasiasa mkongwe na Mwenyekiti wa Chama Cha DP Mch Christopher Mtikila amefariki dunia kwa ajali ya gari kijiji iliyotokea cha Msolwa, Chalinze mkoani Pwani asubuhi ya leo na watu wengine watatu kujeruhiwa katika ajali.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Jafar Ibrahim amethibitisha hilo na kusema watu wengine watatu waliokuwa katika gari hilo wamekimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu.


Gari alilokuwa akisafiria Mtikila

ENDELEA KUTUFUATILIA KWA TAAARIFA ZAIDI

CHANZO: TBC TV

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.