Mwanasiasa mkongwe na Mwenyekiti wa Chama Cha DP Mch Christopher Mtikila amefariki dunia kwa ajali ya gari kijiji iliyotokea cha Msolwa, Chalinze mkoani Pwani asubuhi ya leo na watu wengine watatu kujeruhiwa katika ajali.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Jafar Ibrahim amethibitisha hilo na kusema watu wengine watatu waliokuwa katika gari hilo wamekimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu.
ENDELEA KUTUFUATILIA KWA TAAARIFA ZAIDI
CHANZO: TBC TV
No comments:
Post a Comment