STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 3.10.2015
VIONGOZI wa CCM Zanzibar wamewataka wananchi na wanaCCM wa kisiwa cha Pemba
kuepuka siasa za chuki zilizoanza kurejeshwa tena na wafusi wa chama cha CUF
licha ya kuwa tayari chama hicho kimefanya maridhianao na hivi sasa kimo katika
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa.
Hayo waliyasema viongozi wa CCM Zanzibar katika
Mkutano wa CCM wa Kampeni za uchaguzi uliofanyika huko Kiungoni, Jimbo la Mgogoni
Mkoa wa Kaskazini Pemba uliohudhuriwa na maelfu ya wanaCCM.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai
Ali Vuai Na kusema kuwa CUF kuacha kufanya fujo na vurugu kwani vyama vimesema
vitafanya Kampeni kwa amani na utulivu lakini CUF wameanza kuvunja taratibu
hizo huku akisema kuwa Dk. Shein ametekeleza Ilani kwa zaidi ya asilimia 90
huku akisisitiza kuwa katika suala zima la ajira mipango kabambe imewekwa na
Dk. Shein.
Akiwatambulisha kwa niaba wanachama wa
CUF waliojiunga na CCM wakiwemo Bwana Rashid Mohammed Hassan ameamua kukihama
chama cha CUF Khamis Halfan Khamis pamoja na wenzao kutoka Wete pamoja na
Micheweni.
"uchaguzi wa mwaka huu CUF itapata
kipigo cha paka mwizi kutokana na ushindi mkubwa utakaopatikana na CCM"alisema Vuai.
Vuai aliwatambulisha wanachama wapya
zaidi ya 40 ambao wamejiunga na CCM wakitokea CUF na kueleza kuwa CCM inaposema
itapata ushindi wa asilimia 60 haitanii kwani imefanya maandalizi na vijana
wamekuwa wakiiunga mkono chama hicho kwani wameshautambua ukweli uko wapi.
Vijana hao waliokihama chama cha CUF
walitoa shukurani kwa CCM kwa kuwapokea na kumuhakikishia Dk. Shein kuwa kura
zao zote zitaenda kwa wagombea wa CCM.
Walisema kuwa hivi sasa vijana wameamka na
wamechoka kudanganywa kwani hakuna nchi duniani inayotoa ajira kwa vijana wote wakati
mmoja na kusema kuwa wao wanahitaji kiongozi ambaye atatekeleza Ilani.
Walieleza kushangazwa na mgombea urais wa
CUF anaepita kubadilisha maneno na kuwadanganya wananchi kwa kila anapohutubia
mikutano yake ya kampeni na kumpongeza Dk. Shein kwa kutekeleza Ilani pamoja na
kuishukuru CCM kwa kumsimamisha John Magufuli.
"Vijana wanahitajai serikali ambayo
itakuwa na Ilani ya kuleta maendeleo, na na sio sera za CUF zinazozungumzia
bajeti ya kununulia Pempas"walisema.
Nae Rashid alitoa shukurani kwa mapokezi
makubwa aliyoyapata tokea, Mkoa, Wilaya hadi Wadi kwa lengo la kujiunga na CCM
na kusema kuwa kilichomtoa katika chama cha CUF ni uongo mwingi.
Aidha, anasema CUF walimkataa kwa sababu
alikuwa anashirikiana na CCM na anasema hivi sasa hana cha kufanya kwani
mashamba na vitu vyake vyote vimeharibiwa na wafuasi wa CUF kwa madai kwamba
yeye ni CCM.
Nae Bwana Khamis amesema kuwa ana furaha
kubwa kwa kufika katika mkutano huo wa CCM na kuwaombea dua viongozi na wanaCCM
wote huku akitoa shukurani kwa mapokezi makubwa aliyoyapata na kusema kuwa CCM
anaipenda na imo moyoni mwake.
Nae Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini
Pemba Mberwa Hamad Mberwa alisema kuwa bado wapo wafuasi wa vyama vya upinzani
ambao bado wanaendesha siasa za chuki kisiwani humo ambao wamekuwa wakiwanyima
wananchi bidhaa kwa sababu ya itikadi za kichama.
Alieleza kusikitishwa kwake na hujuma
alizofanyika Bwana Rashid Mohammed baada ya Shamba lake la muhogo kulishwa
ngombe usiku na kuharibu mazao yake yote ya muhogo kwa makusudi pamoja na
kutiwa moto miti yake zaidi ya shamba kwa madai kuwa anawaunga mkono viongozi wa
CCM.
Nae Bi Mauwa Daftari alisema kuwa
mafanikio makubwa katika sekta za maendeleo yamepatikana katika Mkoa huo wa
Kaskazini likiwemo Jimbo hilo la Kojani ikiwa ni pamoja na ujenzi wa
miundombinu ya barabara katika Mkoa huo wa Kaskazini Pemba, huduma za afya,
maji, umeme na nyenginezo.
Alisema kuwa Dk. Shein na John Pombe Magufuli
ni watekelezaji na waadilifu na wala si viongozi vigeugeu kwani wanasema yale
wanayoyaamini pamoja na yale yanayotekelezeka.
Nae Balozi Ali Karume alitumia fursa hiyo
kuwaombea kura viongozi wote wa CCM wakiwemo mgombea Urais wa Zanzibar pamoja
na wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kueleza kuwa Zanzibar imejijengea sifa
kubwa duniani kwa kuwa na amani na utulivu.
"Balozi alikuwa anafanya kazi katika
ubalozi wa Eletria alinieleza kuwa Zanzibar ina bahati kubwa sana kwa kuwa na
amani na utulivu lakini hiyo inatokana na kuwa na kiongozi mzuri anaeiongoza
Zanzibar"alisema Balozi Karume.
Aliwataka Wazanzibari kutodanganywa kwa
kuvunja Muungano na kuona kuwa Muungano ni tatizo na kusema kuwa Zanzibar
imekuwa ikisifika kutokana na amani na utulivu uliopo na kushangwaza na wale
wanaoupinga Muungano.
Balozi Karume alishangazwa na maneno
yanayosemwa na kiongozi wa CUF ya kuigeuza Zanzibar kuwa Singapore ambapo alisema
kuwa kila nchi duniani itaendelea kwa juhudi zake wenyewe kwani kila ndege
anaruka kwa ubawa wake na kusisistiza maneno ya mzee Karume kuwa mtu anatakiwa
asifu chake na mpaka asahau cha mwenzake.
Balozi Amina Salum Ali alisema kuwa
uchaguzi wa mwaka huu ni uchaguzi muhimu kwa Zanzibar na Tanzania nzima kwa
jumla na kueleza kuwa CCM imejijengea
utaratibu mzuri wa kubadilisha wagombea wa urais kwa taratibu na Katiba yao
ilivyoweka lakini CUF haina utaratibu huo.
Alisema kuwa CCM imejipanga vyema na
kugusia kuwa huwezi kudai Mamlaka kamili wakati tayari Mamlaka Kamili yapo na
wanaodai mamlaka hayo hawaelewi wanachokidai.
Alisema kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa
imekuja kwa kutaka amani na utulivu na si vyenginevyo huku akishangazwa na
chama cha CUF kutotaka amani na kuwaeleza vijana vijana kuwa hakuna chama
chengine cha kukiunga mkono isipokuwa CCM
Nae Waziri wa Maji,Ardhi na Nishati
Ramadhani Abdalla Shaaban aligusia suala la mafuta na gesi ambalo limekuwa
likipotoshwa na viongozi wa CUF na kusema kuwa chama hicho kinafanya hivyo kwa
sababu hakina hoja za msingi za kuwaambia wananchi wa Pemba kutokana na
maendeleo makubwa yaliopatikana.
Rajab Mkasaba,
Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment