Na Krantz Mwantepele,
“Huku tupo tu
tunahangaika na kilimo, tunalima kila mwaka,
lakini ukweli ni kwamba kilimo
chetu wala hakina faida basi
tu bora siku ziende”
Lilikuwa ni jibu toka
Alex Jonh maarufu kwa jina la
“Mafuriko” mmoja wa wanaharakati na waraghbishi wa kijiji
cha Lugunga, kilichopo wilaya ya Mbogwe, mkoani Geita
baada ya kuulizwa swali kuhusu maendeleo ya kijiji chao na
mmoja wa waandishi wa habari za mitandao Ali Masoud
maarufu kwa jina la Kipanya.
“Mafuriko” mmoja wa wanaharakati na waraghbishi wa kijiji
cha Lugunga, kilichopo wilaya ya Mbogwe, mkoani Geita
baada ya kuulizwa swali kuhusu maendeleo ya kijiji chao na
mmoja wa waandishi wa habari za mitandao Ali Masoud
maarufu kwa jina la Kipanya.
Kijiji hiki kina wakazi
wanakadiriwa kuwa na wakazi 3,685
wengi wao wakiwa ni wakulima wadogo wadogo. Kilimo
kinaajiri karibu 75% ya wakazi wa vijijini. Lakini ni ukweli
pia, ni kilimo ambacho bado kinategemea jembe la mkono na
mvua na hivyo kuathiri sekta hiyo kwa kiasi kikubwa.
Tukiacha hiyo pia upatikanaji wa pembejeo kwa mifumo
iliyomo kwenye sera ya kilimo, bado ni changamoto kubwa.
wengi wao wakiwa ni wakulima wadogo wadogo. Kilimo
kinaajiri karibu 75% ya wakazi wa vijijini. Lakini ni ukweli
pia, ni kilimo ambacho bado kinategemea jembe la mkono na
mvua na hivyo kuathiri sekta hiyo kwa kiasi kikubwa.
Tukiacha hiyo pia upatikanaji wa pembejeo kwa mifumo
iliyomo kwenye sera ya kilimo, bado ni changamoto kubwa.
Waraghbishi wengi ni
wakulima, ingawa wapo pia walimu,
viongozi wa dini, wenyeviti wa vijiji, na watendaji wa kata
lakini ukweli unabaki kwamba wengi wao wanategemea
kilimo. Changamoto wanazokutana nazo wakulima ndiyo
sababu inayopelekea kilimo kutokuwa cha faida hali
inayowakatisha tamaa na kusema bora liende.
viongozi wa dini, wenyeviti wa vijiji, na watendaji wa kata
lakini ukweli unabaki kwamba wengi wao wanategemea
kilimo. Changamoto wanazokutana nazo wakulima ndiyo
sababu inayopelekea kilimo kutokuwa cha faida hali
inayowakatisha tamaa na kusema bora liende.
Mraghbishi Alex John maarufu kwa jina Mafuriko
akiongea na mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi Herieth Makwetta alipotembelea kijijini hapo .
Akielezea masikitiko yake kuhusu hali yetu, mraghbishi Alex
John ama Mafuriko anasema:
“Ndugu zangu sisi huku
tumesahaulika kabisa, kilimo chetu
tunacholima ni kilimo cha bora liende maana hatuna kabisa
elimu yoyote hapa kijijini. Kila mtu analima na kupanda
anavyojua maana tumeshazoea maisha ya hivi.”
tunacholima ni kilimo cha bora liende maana hatuna kabisa
elimu yoyote hapa kijijini. Kila mtu analima na kupanda
anavyojua maana tumeshazoea maisha ya hivi.”
Katika ufafanuzi wake
Mafuriko ameendelea kusema kuwa
kijiji chao kina ardhi yenye rutuba na inayokubali mazao
mengi yakiwemo mahindi, maharage, mpunga na karanga
lakini licha ya kuwa na ardhi nzuri kama hiyo bado kilimo
hakina faida kwao.
kijiji chao kina ardhi yenye rutuba na inayokubali mazao
mengi yakiwemo mahindi, maharage, mpunga na karanga
lakini licha ya kuwa na ardhi nzuri kama hiyo bado kilimo
hakina faida kwao.
Mchora Katuni Ali Masoud
(mwenye miwani)
akizungumza na waraghbishi na wananchi wa kijiji
cha Lugunga
“Kuna kesi tunakutana nazo ambazo tunazitumia pia kutoa
elimu. Moja ya kesi hizo ni zile na mtu kuacha mifugo yake
bila uangalizi na mwishowe inaingia kwenye mashamba ya
watu na kuanza kula mazao. Utakuta mtu hajui wapi
akapeleke tatizo lake ama akishaikamata mifugo hiyo afanye
nayo ni nini,”
Lakini ni sababu gani
inayowafanya wakose faida katika
kilimo chao licha ya kuwa na ardhi nzuri inayokubali zaidi ya
mazao ya aina tatu. Hapo ndipo waraghbishi walipoanza
kuelezea changamoto wanazokabiliana nazo.
kilimo chao licha ya kuwa na ardhi nzuri inayokubali zaidi ya
mazao ya aina tatu. Hapo ndipo waraghbishi walipoanza
kuelezea changamoto wanazokabiliana nazo.
Akifafanua ukubwa wa
tatizo linalowakabili wakulima wa
kijiji hapo raia mwamilifu na mraghbishi Gabriel Jonathan
anasema:
kijiji hapo raia mwamilifu na mraghbishi Gabriel Jonathan
anasema:
“Unajua ndugu mwaandishi
hapa kijijini tatizo ni moja,
asilimia kubwa ni wakulima na wakulima wengi hawana
elimu. Unaona, wengi wao wameishia darasa la saba na
wengine hawajasoma kabisa, hivyo hata kilimo chao
wanalima ili mradi msimu upite hata akilima heka mbili
akatoa gunia tano kwake anaona sawa.”
asilimia kubwa ni wakulima na wakulima wengi hawana
elimu. Unaona, wengi wao wameishia darasa la saba na
wengine hawajasoma kabisa, hivyo hata kilimo chao
wanalima ili mradi msimu upite hata akilima heka mbili
akatoa gunia tano kwake anaona sawa.”
Ni kweli kilimo ni suala
la kitaalamu na hivyo kuna uhitaji
mkubwa wa ufahamu kwa mkulima, na hapo ndipo serikali
inapomwajiri Afisa Kilimo. Ambaye kimsingi ndio mwenye
jukumu hilo katika kuhakikisha anawatembelea wakulima na
kuwasaidia kitaalamu ili waweze kuzalisha mazao mengi na
yenye ubora.
mkubwa wa ufahamu kwa mkulima, na hapo ndipo serikali
inapomwajiri Afisa Kilimo. Ambaye kimsingi ndio mwenye
jukumu hilo katika kuhakikisha anawatembelea wakulima na
kuwasaidia kitaalamu ili waweze kuzalisha mazao mengi na
yenye ubora.
Hali hii iliibua hamu ya
kutaka kujua iwapo kijijini hapo yupo
Afisa wa Kilimo ama Bwana Shamba kama anavyojulikana na
wengi, katika hali ya kutokuridhishwa na kiwango cha
huduma anachotoa mtaalamu huyo wa mashamba,
mraghbishi Mafuriko alisema,
Afisa wa Kilimo ama Bwana Shamba kama anavyojulikana na
wengi, katika hali ya kutokuridhishwa na kiwango cha
huduma anachotoa mtaalamu huyo wa mashamba,
mraghbishi Mafuriko alisema,
“Bwana Shamba yupo tena
yupo sana lakini hana ushirikiano
kabisa na wakulima wa Lugunga, kwanza hakai hapa kijijini.
Pili wengine hawamjui kabisa yaani kwa wiki anaweza kuja
mara mbili au msimuone mwezi mzima ila mshahara
analipwa”
kabisa na wakulima wa Lugunga, kwanza hakai hapa kijijini.
Pili wengine hawamjui kabisa yaani kwa wiki anaweza kuja
mara mbili au msimuone mwezi mzima ila mshahara
analipwa”
Akiongezea kuhusu upatikanaji
wa Afisa huyo Yohana Julius
alisema:
alisema:
“Tunasikia anaishi
Masumbwe na anapoishi hatujui ni mtaa
gani na wala mimi simjui licha ya kwamba nakaa hapa
katikati (Center) hata nikikutana naye bila kuambiwa simjui
je mwananchi anayeishi Mahameni itakuwaje”
gani na wala mimi simjui licha ya kwamba nakaa hapa
katikati (Center) hata nikikutana naye bila kuambiwa simjui
je mwananchi anayeishi Mahameni itakuwaje”
Mahameni ni kitongoji
kilichopo pembeni ya kijiji cha
Lugunga ambapo pia bwana Shamba wa kijiji hicho
anatakiwa kufika katika kutimiza wajibu wake.
Lugunga ambapo pia bwana Shamba wa kijiji hicho
anatakiwa kufika katika kutimiza wajibu wake.
wenzake wa kijiji cha Lugunga, wakisikiliza maswali
toka kwa
mwandishi
Umbali wa kutoka
Masumbwe hadi Lugunga ni kilometa 17
hali inayodhihirisha kuwepo umbali mrefu kati ya anapoishi
Afisa kilimo huyo Dickson Silvester na kituo chake cha kazi.
hali inayodhihirisha kuwepo umbali mrefu kati ya anapoishi
Afisa kilimo huyo Dickson Silvester na kituo chake cha kazi.
Kukaa tu na kulaumu
hakusaidii sana hivyo ni jukumu la
waraghbishi kujua nini wanachotakiwa kufanya,
waraghbishi kujua nini wanachotakiwa kufanya,
“Mimi naona hapa
tuandamane mpaka ofisi ya Mkurugenzi,
yeye ni mwajiri wake na inawezekana akawa hana hata
taarifa ya nini kinafanyika huku, alisikika mmoja wa
wananchi aliyetambulika kwa jina moja la Hassan.
yeye ni mwajiri wake na inawezekana akawa hana hata
taarifa ya nini kinafanyika huku, alisikika mmoja wa
wananchi aliyetambulika kwa jina moja la Hassan.
Katika hatua nyingine
wananchi hao wakapaza sauti kwa
kumtaka afisa kilimo huyo kurudi kuishi kijijini na kuongeza
kuwa kama alikubali kuja kufanya kazi na kupokea mshahara
basi akubali kuishi katika kijiji hicho cha Lugunga kama
wanavyoishi wananchi alioenda kuwatumikia.
kumtaka afisa kilimo huyo kurudi kuishi kijijini na kuongeza
kuwa kama alikubali kuja kufanya kazi na kupokea mshahara
basi akubali kuishi katika kijiji hicho cha Lugunga kama
wanavyoishi wananchi alioenda kuwatumikia.
Safari ya kujua ukweli
wa kwanini afisa kilimo huyo haishi
katika kituo chake cha kazi ilizidi kusonga mbele na ndipo
mwandishi wa makala hii alipomtafuta kwa njia ya simu na
kufanya naye mahojiano yaliyodumu kwa dakika kumi na
tano.
katika kituo chake cha kazi ilizidi kusonga mbele na ndipo
mwandishi wa makala hii alipomtafuta kwa njia ya simu na
kufanya naye mahojiano yaliyodumu kwa dakika kumi na
tano.
Katika mahojiano hayo
afisa kilimo huyo Dickosn Silvester
alikiri kuwa yeye ndiye afisa kilimo wa kijiji cha Lugunga na
kukanusha taarifa za kuwa haishi katika kituo chake cha kazi.
alikiri kuwa yeye ndiye afisa kilimo wa kijiji cha Lugunga na
kukanusha taarifa za kuwa haishi katika kituo chake cha kazi.
“Mimi ni afisa kilimo wa
Lugunga kweli na ninaishi hapo
hapo Lugunga Center aliyekwambia siishi hapo ni nani?
Mana huo ni uzushi”, alisikika akisema Dickson kwa njia ya
simu wakati akiongea na mwandishi wa makala hii.
hapo Lugunga Center aliyekwambia siishi hapo ni nani?
Mana huo ni uzushi”, alisikika akisema Dickson kwa njia ya
simu wakati akiongea na mwandishi wa makala hii.
Baada ya kupata majibu
ambayo hayakuniridhisha kutoka
kwa afisa kilimo huyo nilirudi Lugunga kwa njia ya simu na
kumtafuta mwenyekiti wa kitongoji cha Lugunga Kati
(Center) bwana Mashiba Dioniz ili kupata ukweli yalipo
makazi ya afisa kilimo huyo.
kwa afisa kilimo huyo nilirudi Lugunga kwa njia ya simu na
kumtafuta mwenyekiti wa kitongoji cha Lugunga Kati
(Center) bwana Mashiba Dioniz ili kupata ukweli yalipo
makazi ya afisa kilimo huyo.
“Mimi ndiye mwenyekiti
wa kitongoji cha hapa Senta,
kwakweli mwandishi huyo afisa kilimo hana makazi hapa
mimi nazijua kaya zangu zote, Ila huwa namuona mara moja
kwa wiki basi ila kusema anaishi hapa ni uongo kabisa.’
Alisema Bwana Mashiba mwenyekiti wa Lugunga.
kwakweli mwandishi huyo afisa kilimo hana makazi hapa
mimi nazijua kaya zangu zote, Ila huwa namuona mara moja
kwa wiki basi ila kusema anaishi hapa ni uongo kabisa.’
Alisema Bwana Mashiba mwenyekiti wa Lugunga.
Lakini waraghbishi hawa
si tu wanajaribu kufuatilia
upatikanaji wa huduma za ugani katika kijiji chao, ila
wameendelea kutoa elimu kwa wanakajiji wengine wa kijiji
hapo. Mfano mmoja ni migogoro baina ya wakulima
wenyewe. Na kwa kuwa waraghbishi hawa hawaitishi
mikutano ya vijiji mara nyingi wamekuwa wakitumia maeneo
ya migogoro kama sehemu yao ya kutolea elimu.
upatikanaji wa huduma za ugani katika kijiji chao, ila
wameendelea kutoa elimu kwa wanakajiji wengine wa kijiji
hapo. Mfano mmoja ni migogoro baina ya wakulima
wenyewe. Na kwa kuwa waraghbishi hawa hawaitishi
mikutano ya vijiji mara nyingi wamekuwa wakitumia maeneo
ya migogoro kama sehemu yao ya kutolea elimu.
Akifafanua hilo Felix
Daudi, mraghbishi mwingine katika
kijiji hicho anasema,
kijiji hicho anasema,
“Kuna kesi tunakutana nazo ambazo tunazitumia pia kutoa
elimu. Moja ya kesi hizo ni zile na mtu kuacha mifugo yake
bila uangalizi na mwishowe inaingia kwenye mashamba ya
watu na kuanza kula mazao. Utakuta mtu hajui wapi
akapeleke tatizo lake ama akishaikamata mifugo hiyo afanye
nayo ni nini,”
Hivyo ni vizuri watendaji
wa serikali wakashirikiana na
waraghbishi na muda mwingine kuwapatia ujuzi mdogo
mdogo. Hii itasaidia kufanikisha shabaha ya Maendeleo
kwani pande zote watakuwa wanategemeana. Na si katika
hali hii ambayo watu wanashutumiana. Hivyo ni jukumu letu
sote kucheza nafasi zetu katika kusukuma gurudumu la
maendeleo.
waraghbishi na muda mwingine kuwapatia ujuzi mdogo
mdogo. Hii itasaidia kufanikisha shabaha ya Maendeleo
kwani pande zote watakuwa wanategemeana. Na si katika
hali hii ambayo watu wanashutumiana. Hivyo ni jukumu letu
sote kucheza nafasi zetu katika kusukuma gurudumu la
maendeleo.
Moja ya mashamba ya
mpunga yaliyopo katika kijiji cha Lugunga
No comments:
Post a Comment