Habari za Punde

Fastjet yatuma salamu za Rambirambi kwa kifo cha Mkurugenzi Mkuu wa wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, hayati Mhandisi Suleiman S. Suleiman.

Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa  wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, hayati Mhandisi  Suleiman S. Suleiman.  


SALAMU ZA RAMBIRAMBI

Dar es Salaam, 19 Januari, 2016

Uongozi na wafanyakazi wa Fastjet Tanzania  umepokea kwa masikitiko makubwa  taarifa za  kifo cha ghafla cha Mkurugenzi Mkuu wa  wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, hayati Mhandisi  Suleiman S. Suleiman.

Tunaungana na familia, marafiki, ndugu, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania kutuma salamu za rambirambi katika kipindi hiki cha kuomboleza.

Fastjet Tanzania imefanyakazi kwa ukaribu na Mhandisi Suleiman na tunatambua mchango wake katika kukuza sekta ya usafiri wa anga nchini.

Tutaukosa kwa kiwango kikubwa ushauri, uongozi na ushauri wake kutokana na kifo chake.

Tunaomba roho yake ipumzike kwa amani peponi.

Amin.
Imetolewa na Meneja Mkuu wa fastjet Tanzania, John Corse.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.