Habari za Punde

ZEC Yaendelea na Matayarisho ya Uchaguzi wa Marudio Machi 20.

Na.Mwandishi Wetu.
Tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC imesema maandalizi ya uchaguzi wa marudio wa tarehe 20 marchi 2016 yamefikia hatua nzuri na  kazi ya uchapishaji wa daftari la wapiga kura itakuwa imekamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi huu.
Taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Tume hiyo Mhe.Jecha Salim Jecha imesema kuwa madaftari ya wapiga kura yatakuwa nje ya vituo yatabandikwa wiki moja kabla ya uchaguzi  ili kuwapa nafasi wapiga kura kuelewa vituo walivyopangiwa.
Ameyataja matayarisho mengine yaliyokuwa katika hatua nzuri kuwa ni pamoja uteuzi wa wasimamizi wa Majimbo, upangaji wa vifaa na vituo, pamoja na mafunzo kwa watendaji.
Mhe.Jecha ameongeza pia  matayarisho ya awali ya uchapishaji wa karatasi za kura yamekamilika baada ya tume kumpitisha mchapishaji wa karatasi hizo na zinatarajiwa kuwasili nchini mwanzoni mwa mwezi wa Marchi.
Akizungumzia mawasiliano kwa vyama vya siasa na wagombea Mhe.Jecha amesema kuwa tume itaendelea kuwahesabu wagombea wote wa uchaguzi uliopita ni halali kutokana na kutofuata utaratibu wa kisheria za  kujitoa kwa wagombea.
Ameeleza kuwa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi nambari 11 ya mwaka 1984 sura ya tatu kifungu cha 31 hadi 37a kinatoa sharti la kuwepo wadhamini wa wagombea na hakuna Chama kilichoiandikia tume kuwa kimefuta udhamini wa wagombea wake kushiriki katika uchaguzi huo.

1 comment:

  1. Kwakweli mimi si mshabiki wa chama chochote cha siasa ila kwa mtazamo wangu uchaguzi wa March 20-2016 utakuwa haauna mvuto na wakulazimisha, lingekuwa jambo la busara sana kama vyama vikuu vya siasa yaani Cuf na Ccm kukaa pamoja kuliangalia upya hili suala kwa maslahi ya wazanzibari kwa ujumla.
    Wangekubaliana kwanza hii tume ibadilishwe na Mh Jecha angekaa pembeni kwaani waZanzibar wengi wamekuwa hawana imani nae hata ukiangalia CCM wenyeewe walikuwa hawamtaki seuze sasa karudi kwa kasi mpya ya uchaguzi wa marudio?
    Uchaguzi huu ukimalizika bila shaka utatawaliwa na ulipizaji visasi na vya kushtukizia baaina ya wafuasi wa vyama viwili vikubwa.
    Mtazamo wangu kwa serekali ya SMZ na wadao woote kwa pamoja wakae chini na kufikiria upya uchaguzi wa marudio kuliko kutupeleka zanzibar kule tulipotoka kwa utashi wa vyama na uroho wa madaraka.

    Zanzibar ni njema atakae na aje.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.