Habari za Punde

TFM Yatoa Elimu kwa Waandishi wa Habari Kisiwani Pemba.

Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari Pemba Saidi Moahmed Ali, akifungua mkutano wa waandishi wa habari juu ya ujazaji wa fomu za maombi kwa Tanzania Media Foundation, uliofanyika katika ukumbi wa Makonyo Wawi. 
Waandishi wa habari kisiwani Pemba, kutoka vyombo mbali mbali vya habari wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Pemba Press Club, wakati alipokuwa akifungua mkutano wa siku moja ulioandaliwa na Tanzania Media Foundation
 Afisa Miradi kutoka Tanzania Media Faoundation Alex Kanyambo, akizungumza na waandishi wa habari kisiwani Pemba juu ya TMF mpya na miradi yake kwa kipindi hiki
Mwandishi wa Habari kutoka shirika la Utangazaji ZBC-Radio Pemba, Mchanga Haroub akiuliza swaji juu ya uombani wa maombi kwa taasisi za kihabari
Waandishi wa habari Radhia Abdalla wa Zenj FM na Salama Omar wa Swahiba FM, wakizungumza na Afisa Miradi wa TMF Alex Kanyambo mara baada ya kumaliza kwa mkutano na waandishi wa habari huko katika ukumbi wa Makonyo Wawi Chake Chake
Waandishi wa habari kisiwani Pemba wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Tanzania Media Foundation (TMF)mara baada ya kumaliza kwa mkutano wa siku moja juu ya Ujazaji wa fomu ya maombi kwa njia ya Mtandao.
(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.