Habari za Punde

Maalim Seif Alazwa Hospitali ya Hindu Mandal Dar.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na waandishi wa habari katika hospitali ya Hindu Mandal Jijini Dar es Salaam kuelezea maendeleo ya afya yake. Amesema anaendelea vyema baada ya jana kuugua ghafla na kulazwa katika hospitali hiyo. Amewashukuru wananchi ndani na nje ya nchi kwa kuonesha mapenzi na mashirikiano makubwa. Anatarajiwa kutoka hospitalini hapo leo jioni (Picha na Salmin Said, OMKR)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.