Na Mwandishi
wetu, Pemba
AFISI ya
Mkurugenzi wa Mashitaka Pemba, imekiri kuwa jalada la watuhumiwa 10, akiwemo aliekuwa Mwakilishi
wa Jimbo la Kiwani Hija Hassan Hija, wameshalipokea kutoka Polisi na
wanaendelea kulipitia mstari kwa mstari, ili wajiridhishe kabla ya kuliombea
kibali ili lipelekwe mahakamani.
Afisi
hiyo imesema, jalada hilo limetua afisini mwao, tokea Julai 11, mwaka huu, na
baada ya kazi wanayoendelea nayo watalisafirisha hadi kwa Mkurugenzi wa Afisi
hiyo Kisiwani Unguja, ili kuliombea kibali kabla ya kulipandisha mahakamani.
Mwanasheria
Dhamana wa afisi hiyo kisiwani Pemba Al-baghiri Yakut Juma, alisema wao
wanapokea majalada kadhaa ya kesi, huwa hawakurupuki kuyapandisha mahakamani,
kwani sheria zainawaruhusu kwanza kuyapitia, ili waone kama kuna uhusiano wa
kesi na kilichomo ndani ya jalada husika.
Alieleza
kuwa, majalada ya tuhuma kama za uchochezi na fumanizi baada ya wao kuyapatia
kwa pamoja, huyapeleka Unguja kwa mkuu wao wa kazi, ili kuyaombea kibali maalum
na kisha ndio wapande nayo mahakamani.
“Kwanza
ni kweli jalada lenye watuhumiwa kadhaa akiwemo Hija Hassan Haji, Seif Khamis
Mohamed, Hamad Mussa Rashid, Simai Mcha Khamis, Khatib Haji Dadi, Abdalla Ali,
Mussa Seif Massoud tumelipokea tokea tarehe 11 mwezi huu na tunaendelea nalo
kulipitia kwa umakini’’,aliweka wazi.
Aidha
mwanasheria huyo dhamana wa afisi ya Mkurugenzi wa mashitaka Pemba, aliwataka
wengine waliomo kwenye jalada hilo kuwa ni Rashid Ali Hamad, Juma Abdalla
Khatib, Mohamed Ame Ussi na Maulid Issa Salim ambapo alisema baada ya taratib
kukamilika hatua nyengine zitafuata.
Hata
hivyo alisema afisi yake wala Jeshi la Polisi, halipo kwa ajili ya kuwaonea
wananchi na wamekuwa wakifanyakazi kwa kushirikiana ili haki itendeke katika
kuwahudumia wananchi.
“Wananchi
wasiwe na hofu wala wasisi, kwamba eti sisi na Jeshi la Polisi tutamuonea mtu
hapana, tunafanyaka kazi kwa mujibu taratibu na sheria na ndio maana, jalada
lipo kwetu ili kuangalia zaidi kisheria’’,alieleza.
Awali
Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba, Shehan Mohamed Shehan alisema kuwa,
tayari jalada la watuhumiwa kadhaa akiwemo Hija Hassan Hija wameshalifikisha
kwa DPP, kwa ajili ya kwenda mahakamani.
Nilisikia
kuwa wenzetu wa DPP wanaendelea kulipitia jalada hilo, na naamini wanafanya
kazi zao kwa sheria na taratibu, na wananchi wawe watulivu, sheria
zinafanyakazi ili hali itendeke.
Wakati huo huo Kamanda wa Polisi mkoa wa
kaskazini Pemba Hassan Nassir, alisema Jeshi lake halijamshikilia wala kumuhoji
aliekuwa mwakilishi wa Jimbo la Gando Said Ali Mbarouk kama taarifa
zilivyozagaa mitaani.
Alisema
kwa sasa mkoa wake ni shuwari na wanaendelea na doria na kuwataka wananchi
kuendelea kushirikiana ili kulinda hali ya amani na utulivu mkoani humo.
Katika hatua nyengine, taarifa zilizopatikana zinaeleza kuwa
Jeshi la Polisi mkoani humo, limefanikiwa kuwatia mikononi, watuhumiwa watatu
wakidaiwa kuwabakaji watoto wanne akiwemo pia mlemavu mmoja wa akili.
Matukio hayo ambayo yanamuhusisha mtuhumiwa Khamis Sief
Khamis (35) mkaazi wa Limbani aliwabaka watoto wawili baina ya Julai 1 na 10
mwaka huu.
Tukio la kwanza linamlomkabilia mtuhumiwa huyo lilitokea
Julai 1 mwaka huu, majira ya saa 6: 30 mchana ndani ya mwezi mtukufu wa ambapo
ilidaiwa alimbaka mtoto (8).
Aidha Jeshi hilo pia linamshikilia kijana huyo huyo kwa kosa
kama hilo, ambalo alidaiwa kulitenda Juali 10 kwa kumbaka mtoto mwengine
(6).
Mtuhumiwa mwengine aliekamatwa na jeshi hilo kwa tuhuma
kumuingilia kwa nguvu mwanamke (35) mwenye ulemavu wa akili mkaazi wa Wete,
tukio lililotokea Julai 7 majira ya saa 2:00 asubuhi.
Mmwengine aliemikononi mwa Jeshi la Polisi akikabiliwa na matukio mawili ni Nassor Issa
Nassor (26) kwa tuhuma za kumbaka watoto wawili mmoja (3) na mwengine (8).
Juzi
Julai 12, mahakama ya wilaya ya Chakechake, iliwapa dhamana watuhumiwa 26 wa
makosa mbali mbali yakiwemo ya ukataji na ung’oaji wa mikarafuu 174, mihogo,
migomba na wanatarajia kurudi tena mahakamani hapo Julai 26, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment