Na Salmin Juma -Pemba
Mataifa mbalimbali duniania yamekubali kutia saini mitakaba ya “haki za binaadamu”kupitia
umoja wa mataifa UN ambazo kwa namna
moja ama nyengineyo zitapelekea kua na maisha bora kwa kila raia wake, moja
miongoni mwa mataifa hayo ni Tanzania, kupitia
mikataba hiyo imeridhia na kukubali kulinda na kuhifadhi haki za binaadamu
ikiwemo ya kuishi,elimu na nyenginezo na haki hizo pia zinapatikana katika
katiba yake ya 1977 na ile ya 1984 ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ).
Katika kulinda haki hizo
michakatombalimbali tumekua tukishuhudia nchini mwetu ikitekelezwa ili kuhakikisha kila raia anajua
haki zake kama binaadamu,miongoni mwa hatua hizo ni utoaji wa elimu kwa
wananchi unaoendelea kutolewa na taasisi mbalimbali za kiserikali na za
kibinafsi.
Ingawa zipo nyingi sana lakini hapa
inafaa kukipongeza kituo cha huduma za sharia Zanzibar (ZLSC) tawi la Pemba, wamekua wakishuhudiwa kupita kila kona ya visiwa vya
Pemba, shehia baada ya shehia kutoa
elimu kwa wananchi pamoja na uwendeshaji mafunzo maalum juu ya uwelewa wa haki
hizo wanazotakiwa kuzipata, kanakwamba haitoshi pia kituo hicho kinashuhudiwa
wakiendesha vipindi tofauti katika luninga (radio) wakizungumzia haki za
kibaadamu, kuzilinda na kuzihifadhi.
Licha ya kua juhudi ya usambazaji
elimu juu ya dhana hii ni kubwa lakini
bado inaonekana kuna baadhi ya raia hawajanufaika kabisa na elimu hiyo
ukizingatia haki kubwa mojawapo ni “haki
ya kuishi tena katika mazingira yaliyobora” lakini bado kuna raia wa kitanzania
wanakosa na wanaendelea kukosa haki hiyo, bado wanaishi katika maisha ya dhiki,
dhihaka na ya kudhalilika, yaliyosababishwa na ukosefu wa elimu baina ya
wanajamii wenyewe.
Jicho la mwandishi wa makala hii lilihuzinika na kupigwa
na butwaa baada ya kushuhudia hali mbaya
ya maisha yanayomkabili Mwadhanije
Hamadi kutoka kijiji cha Tondooni
Makangale Wilaya ya Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba.
Mwadhanije ni kijana mdogo wa miaka
19, mpaka naandika makala hii bado hajui nini maisha bora, na hii imesababishwa
na aliyekua mumewe mara tu baada ya kuingia katika ndoa. Kijana huyu aliishi
katika maisha ya umasikini tangia alipozaliwa kijijini kwao hapo, familia yake
haikua yenye kujipata kimaisha kama
zilivyo baadhi ya familia nyengine nchini, ingawa hali haikua hali lakini
alistahamili kuishi mpaka pale wazee walipoamua kumpa mume. Aliingia katika
ndoa kwa furaha na amani akiamini maisha yatakua mazuri na alizidi kupata
matumaini pale alipokua akipokea ahadi
kemkem kutoka kwa mtarajiwa wa ndoa yake.
Mwezi wa 09/2015 rasmi aliolewa na bw:
Ali Jabir na kuishi huko huko Tondooni Makangale Pemba, maisha yalikua mazuri
ya kusikizana katika miezi mitatu ya mwanzo, kila mmoja alimuona mwenzake ndie
wake katika kila jambo maishani.
Misukosuko na mikasa ilijitokea punde
tu baada ya kupata ujauzito, wataalamu wa afya ya mwanaadau wanatueleza kua, mara
nyingi mwanamke anapokua katika hali ya ujauzito hubadilika katika halitofauti (kama
vile kumchukia mume,kuchagua vyakula,kukerwa na baadhi ya harufu n.k) hapa
ndipo mambo yalipoanzia.
Nilibahatika kunzungumza na mama wa
Mwadhanije Bi Mbikau Kombo Hamadi alionesha hali ya masikitiko makubwa kutokana na misukosuko ya ndoa ya binti yake,
alisema ndoa hiyo haikua na amani hata kidogo kwa sababu hata uyo mume walikua
hawamtaki isipokua baba mzazi ndio alieifanya harusi hiyo.
Wakati namzungumza na mama wa kijana
huyo ilikua ni mwezi wa 05/2016 ambapo tayari Mwadhanije alishaachika, ndoa yao
takriban ilidumu kwa muda wa miezi 9.
Msomaji wa makala hii napenda
kukwambia bayana kua hutoona mazungumzo baina yangu na Mwadhanije mwenyewe ni
kwasababu ya kua ni mgonjwa wa akili (pungufu) pia hawezi kuzungumza hata
kidogo (Bubu)
Bi Mbikau alizidi kueleza kua, hali
ya mototo wao waliijua mapema na waliamua kumueleza (muowaji) hali halisi
ilivyo baada ya baba mzazi kutaka
kumuozesha na walizidi kupata matumaini kwa sababu bw:Jabir alikua(aliyekua
mumewe) ni mkaazi wa hapo hapo kijijini alimfahamu fika Mwadhanije na hali yake
ilivyokua, aliahidi kuishi nae hivyohivyo na kweli alitimiza ahadi yake ingawa
haikua dumu daima uzalendo ulianza kumshinda pale alipoona hali yake kubadilika
baada ya ujauzito,kama maneno ya daktari yalivyofahamisha ndivyo hali ilivyokua
kwa Mwadhanije Hamadi dhidi ya mumewe Jabir ilifikia hatua mpaka unyumba alinyimwa, nguo za kazini kuchwanwa, chakula
kutoekea tena kama ilivyo kawaida.
Sikutaka kuishia hapo nilijaribu
kudadisi kwa undania kutaka kujua kwanini aliamua kuchukua uwamuzi wa kumuacha
mkewe huyo ambae hata kuongea hawezi na akili zake zimempungua pia ukizingatia
ni mjamzito, alisema amechoshwa na vitendo vyake hasa kwakua kila apelekapo
malalamiko wa wazee wake haoni lolote linalotendeka kama msaada kwake.
Katika hali ya kuhuzunisha Ali Jabir
anaamini Mwadhanije ndie aliemkataa wala sio yeye “hata kulala aliondoka hapa
akawa analala kwa mamaake, kamba zangu za kupandia minazi amezikata zote, kila
kitu changu amekiharibu hata tandiko tulilokua tunalalamia amelichanachana
lakini kila nikishitaki kwa wazee wake hakuna wanalonifanyia hapo mimi ndio
nikaamua kumuacha kwasababu kanikataa mwenyewe”alisema Jabir.
Hali bado ni ya kuumiza kwa wazazi wa
Mwadhanije wamesema wanaumia sana kuachwa kwa mototo wao na mengi sana
waliyaeleza mbele ya mwandishi, baba mzazi ambae ni bw:Hamad wa Hamad alisema
hakuridhika hata kidogo na tuko hilo kwani mtoto wao haachiki kwakua ni
mpungufu wa akili “akili za mtoto kama unavyoziona haachiki yule”alisema Hamad
Madai mengine wanayoyadaiwa na
wanafamilia hao ni kua, kuna haki zake bado hajarudishiwa kama ikiwamo kitanda na godoro kwakua ndivyo vilivyokua
mahari yake wakati alipoolewa sambamba na kutohudumiwa huduma yoyote na
alieyekua mumewe. Katika kulifatilia hili uchunguzi uligundua ni kweli hakuna
chochote katika mahari yake alichorudishiwa na bwana Ali Jabir.
Wakati nazungumza na wazazi wa kijana
huyu nilishuhudia hali ya afya ya Mwadhanije ikiwa dhoofulhali baada ya kuuliza
nilijibiwa kua ujauzito wa miezi mitano (5) na siku kadhaa aliyokua nao ndio
unaomsumbua na kumuhilikisha namna hiyo.
Bi Zuwena Swaleh Ali ni mratibu
wa wanawake na watoto na mwanamtandao wa
wanawake wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba amethibitisha kutokea mkasa huo shehiani mwake
huku akisema kua aliwahi kumtafuta aliyekua mumewe na kumtaka kurudisha mahari ya
kijana Mwadhanije lakini Jabir alikataa katakata kurudisha chochote katika mahari.
Wakati tuyanzungumza haya Mwadhanije
alikua pembeni yetu hali yake si ya kuridhisha hata kidogo, amewiva kwa ujanjano
ngozi yake, miguu ilimvimba pamoja na uso wake, la kusikitisha ni kua alikua
peke yake lakini sasa ana mwenzake tumboni na hali kama inavyojieleza unafikiri
nini kinakuja mbele yake katika mazingira kama haya.
Aidha tulipata bahati ya kuzungumza
na Bi Mize wa Bimize afisa wa wanawake na watoto Wilaya ya
Micheweni kutoka Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Vijana Wanawake na Watoto alifahamisha kua,kesi hiyo ipo ingawa juhudi
za kunusuru ndoa hiyo zinaendelea lakini bado inaonekana kua na ugumu ndani
yake ni kutokana na kutokuwepo kwa mashirikiano ya kutosha kwa wahusika wa
tukio hilo.
Kupitia tukio la kijana huyu, inabainika wazi kua ni elimu inayotolewa inaonekana bado haijatosheleza
kwa baadhi ya wananchi juu ya haki za binaadamu, ni kwamba yote yaliyombele ya
kijana huyu yalisababishwa na kuvunjiaka kwa ndoa, hata ukitazama sababu
zenyewe utagundua kua ni kutokua na elimu tu ya jinsi gani utaishi na mtu kama
Mwadhanije, jinsi gani utanishi na mwenye ujauzito.
Kutokana na kutokua na elimu ya
kutosha imepelekea mpaka muda huu Mwadhanije kukosa haki ya msingi ya
kibinaadamu “haki ya kuishi katika maisha bora” hali yake ni dhaifu ya
kutazamaiwa.
Kila mmoja ni shuhuda nambari moja wa
matukio yaliyotanda nchini mwetu ya kuhilikishwa na kunyanya kingono wasichana
wasiokua na hatia mfano mzuri wale wenye akili timamu,jee kwa Mwadhanije
tunamtazama vipi katika mazingira kama haya.
Hujudi bado inahitajika kwa upande wa
serikali ,wadau na watetezi wa haki za raia tulitazame hili kwa jicho la
huruma,ndoa imeshatenguka ingawa kuna michakato ya kuirudisha tena kama
ilivyokua lakini bado inaonekana kuna ugumu wa kufikia lengo hilo.
Kubwa zaidi hapa ninalopenda
kulifikisha kwa wadau tujali afya ya Mwadhanije lakini hasa kile kiumbe kilichopo
tumboni ambacho kina siku chache tu kuja
duniani maandalizi yake yanahitajika tokea leo nini kinafanyika kwa kunusura
hali ya maumivu kuzidi kumuandama msichana huyu?
0772997018
No comments:
Post a Comment