Habari za Punde

Changamoto katika biashara ya Utalii zinavyowaathiri wawekezaji wazawa Pemba

 MENEJA wa Hoteli ya Mbuyu Mkavu iliyoko Vitongoji Wilaya ya Chake Chake, Abdalla Said ambaye ni muwekazaji mzalendo wa ndani, akieleza matatizo yaliyopelekea kuifunga hoteli yake, katika kikao cha pamoja na viongozi wa kamisheni ya Utalii Pemba, wa kwanza kulia ni mdhamini wa kamisheni hiyo Suleiman Amour Suleiman.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).
 SEHEMU ya kupatia chakula wageni wanaofika katika hoteli ya Mbuyu Mkavu iliyoko Vitongoji Wilaya ya Chake Chake Pemba, hoteli hiyo kwa sasa imefungwa kutokana na changamoto za umeme kutokuwepo hotelini hapo.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).
 IPO haja kwa watembeza watalii Kisiwani Pemba, kuwafahamisha wageni wao jinsi wanavyotakiwa kutembea kwa kufuata mila na silka za wananchi wa kisiwa cha Pemba, pichani watalii wakiwa katika mji wa chake chake bila ya kujistiri katika miili yao.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).
MDHAMINI wa Kamisheni ya Utali Kisiwani Pemba, Mwalimu Suleiman Amour Suleiman wa kwanza kulia, akikagua buku la wageni katika moja ya hoteli za kitalii zinazolaza wageni ndani ya Wilaya ya Chake Chake.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.