Habari za Punde

Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Afisi ya Rais azungumza na waandishi wa vyombo vya FM kuhusu kongamano la Diaspora

 Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Nd,Salum Maulid Salum (katikati) akizungumza na waandishi wa Habari wa vyombo mbali mbali vya Redio za FM kuhusu kongamano la Watanzania wanaoishi Nje ya Nchi (Diaspora) linalotarajiwa kufanyika  Agosti 24 mwaka huu,[Picha na Ikulu.] 02/08/2016.
 Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Nd,Salum Maulid Salum (wa pili kulia) alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali vya Redio za  FM kuhusu kongamano la Watanzania wanaoishi Nje ya Nchi (Diaspora) linalotarajiwa kufanyika  Agosti 24 mwaka huu (kushoto) Naibu Katibu wa Rais Nd,Marium Haji Mrisho na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Silima Kombo Haji,[Picha na Ikulu.] 02/08/2016.
Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Nd,Salum Maulid Salum (kulia) alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali vya Redioza  FM kuhusu kongamano la Watanzania wanaoishi Nje ya Nchi (Diaspora) linalotarajiwa kufanyika  Agosti 24 mwaka huu (kushoto)   Mkurugenzi wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Silima Kombo Haji,[Picha na Ikulu.] 02/08/2016.


STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                          2.8.2016
---
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zinatambua mchango mkubwa wa Wanadiaspora na ndio maana hutayarisha makongamano ambayo hutoa fursa ya kujadili masuala mbali mbali ya kimaendeleo kwa lengo la kuimarisha uchumi wa Tanzania na ustawi wa wananchi wake.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na  Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Salum Maulid Salum aliyasema hayo leo huko Ikulu Mjini Zanzibar wakati alipofanya mazungumzo na waandishi wa Habari mbali mbali kutoka Redio za FM zinazofanya kazi zake hapa Zanzibar kuhusu Kongamano la Diapora la Tanzania linalotarajiwa kufanyika hapa Zanzibar mwaka huu.

Katika maelezo yake Katibu Mkuu huyo aliyekuwa pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Silima Kombo Haji, alisema kuwa kwa miaka miwili iliyopita makongamano hayo yamefanyika  Dar-es-Salam na kusisitiza kuwa mikutano iliyokwisha fanyika imeweza kuleta mafanikio makubwa.

Alisema kuwa Mkutano wa mwaka huu unatarajiwa kufanyika hapa Zanzibar kwa muda wa siku mbili kati ya tarehe 24 na 25 linatarajiwa kufunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na kufungwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli huko katika ukumbi wa hoteli ya  Zanzibar Beach Resort.

Katibu Mkuu huyo alisema kuwa mada mbali mbali zinatarajiwa kutolewa katika Kongamano hilo ambalo  kauli mbiu yake ya kila mwaka ni “Mtu kwao ndio Ngao’ ambapo pia, ujumbe mkubwa kwa mwaka huu ni “Mtizamo mpya wa Kuimarisha Utalii wa Tanzania na uekezaji”.

Katika melezo yake Katibu Salum alisema kuwa tayari matayarisho ya kongamano huo yanaendelea vizuri na kueleza kuwa Wanadiaspora wamekuwa na mwamko mkubwa katika ushiriki ambapo kila mwaka idadi ya ushiriki wao imekuwa ikiongezeka huku akieleza kuwa vyombo vya habari zikiwemo Redio za FM, vina nafasi kubwa katika kuwaeleza wananchi juu ya mkutano huo.

Aidha, alisema kuwa miongoni mwa mafanikio yaliopatikana ni pamoja na Wanadiaspora wengi wa hapa nchini wameweza kutoa michango yao mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuimarisha mirado mbali mbali ya maendeleo ikiwemo ya afya, elimu na mengineyo.

Katibu Mkuu huyo alitumia fursa hiyo kueleza juhudi za viongozi hapa nchin i katika kuhakikisha suala hilo linaimarika huku akitolea mfano juhudi za makusudi zinazochukuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein katika kuhakikisha ushirikiano kati ya Wanadiaspora na Serikali zote mbili unaimarika.

Nae Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Silima Kombo Haji aliwaeleza waandishi hao wa habari faida zinazopatikana kutokana na kuunganishwa kwa Wanadiaspora hapa nchini pamoja na changamoto zilizopo.

Balozi Silima alizitaja baadhi ya nchi zilizopo ndani na nje ya Afrika ambazo zimenufaika na zinazaendelea kunufaika kutokana na Wanadiaspora wa nchi zao zikiwemo Kenya, Ethiopia, Ghanam Idia, Pakistan, Ufilipino, Bangladesh na nyenginezo.

Sambamba na hayo, Balozi Silima alisema kuwa serikali zote mbili zimeweka mikakati maalum ya kuhakikisha Wanadiaspora wanapewa kipaumbele sambamba na kushirikishwa katika masuala mbali mbali ya maendeleo kwa nchi yao.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.