Viongozi wakiwa katika meza
kuu wakati wa ufunguzi wa Kongamano hilo .
Mgeni rasmi Mheshimiwa Rashid Ali Juma (wa tatu kulia), Waziri wa Habari,
Michezo, Utamaduni na Sanaa akibadilishana na Bwana Abdalla Mwinyi Khamis
(aliyevaa kofia), Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi mstaafu.
Mheshimiwa mgeni rasmi, viongozi mbali mbali na
washiriki wa Kongamano wakati wa zoezi la kupandisha bendera za nchi wanachama
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuashiria ufunguzi rasmi
Washiriki wa Kongamano kutoka
mataifa wanachama wa CHAWAKAMA.
Chuo Kikuu cha Taifa
cha Zanzibar (SUZA) kimekuwa mwenyeji wa Kongamano la 12 la Chama cha Wanafunzi wa Kiswahili wa Afrika
ya Mashariki (CHAWAKAMA) ambalo limeanza tarehe 21 Septemba, 2016 na
kufunguliwa na mgeni rasmi Mheshimiwa Rashid Ali Juma, Waziri wa Habari,
Michezo, Utamaduni na Sanaa. Kongamano hili ambalo litafungwa tarehe 23
Septemba, 2016 linafanyika katika ukumbi wa jengo la zamani la Baraza la
Wawakilishi ambao sasa ni la Wizara ya Habari, Michezo, Utamaduni na Sanaa.
Katika Kongamano hili lenye kauli mbiu “Kiswahili
chako, fursa yako” linaambatana na utoaji wa mada kutoka kwa wataalamu mbali
mbali wa lugha ya Kiswahili na kuwa na majadiliano yanayohusu lugha ya
Kiswahili pamoja na mila, silka, tabia, desturi na utamaduni unaoambatana na
lugha hiyo.
No comments:
Post a Comment