Habari za Punde

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg. Vuai Ali Vuai Azinduzi wa Ujenzi wa Ukuta wa Jengo la Ofisi ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja Eneo la Tunguu Zanzibar.

Michoro ya Jengo la Kitega Uchumi la Afisi ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja linalotarajiwa kujengwa katika eneo la Tunguu Zanzibar likiwa na gorofa 15. Likiwa na  sehemu za biashara na makaazi ya Watu na Ofisi. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai akisalimiana na Viongozi wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja wakati akiwasili katika viwanja vya ujenzi huo hapo tunguu kwea ajili ya uzinduzi wa ujenzi wa ukuta wa jengo hilo la Kisasa la CCM kwa Mkoa wa Kusini Unguja.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akisalimiana na Viongozi wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai akiwasili katika viwanja vya Tunguu Unguja kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa uzio wa ukuta wa Jengo hilo huko tunguu Wilaya ya Kati Unguja.
Katibu wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja Bi Sauda akitowa maelezo kwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar wakati alipofika katika eneo hilo la ujenzi wa Afisi Kuu ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja katika eneo la Tunguu Zanzibar.
Vijana wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja wakishiriki katika kuchimba msingi wa ujenzi wa ukuta wa Mradi wa Jengo la Afisi ya CCM Mkoa wa Kusini Unguja.
Vijana wakishiriki katika ujenzi wa taifa wa uchimbaji wa msingi wa ujenzi wa ukuta. 









No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.