Habari za Punde

Polisi yamtia mbaroni askari aliechukua rushwa kutoka kwa raia wa kigeni


Jeshi la Polisi Zanzibar limemkamata askari wake anayetuhumiwa kupokea rushwa kutoka kwa raia wa kigeni baada ya kumkamata kwa kosa la barabarani na kumuachia huku akimuahidi kumlinda.

Uamuzi huo wa jeshi la polisi Zanzibar umetolewa na kamishna mkuu wa jeshi hilo hapa Zanziabr CP Hamdan Omar Makame wakati akiongea na waandishi wa habari katika makao makuu ya polisi ambapo amesema jeshi la polisi limesikitishwa sana na kulani kitendo hicho cha askari huyo akipokea rushwa kwa kosa la raia huyo kutovaa mkanda na kitendo hicho kusambazwa kwenye mitandao ambapo amemtaja askari huyo ni sajeti Talib Hamad na siyo jina la Ali huku pia akisema kitendo hicho kilifanyika Mkokotoni na sio Mahonda kama alivyokaririwa askari huyo kwenye mahojiano ya mtandao.

Kamishna mkuu huyo wa polisi Zanzibar amesema kwa sasa askari huyo atachukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa taratibu za kipolisi na ikithibitika kuwepo kosa la jinai atapelekwa kwenye vyombo vya sheria vya dola huku na akisisitiza wananchi waendelea kutoa ushirikiano.

Kwa mujibu wa tukio hilo lilivyoonekana kwenye mtandao huo raia huyo alikamtwa kwa kosa la kutovaa mkanda wa gari na askari huyo aliamua kuchukua leseni ya barabara na kumuhakikishia kuwa aendele na safari na atamlinda huku akionekana akipokea fedha taslimu.


1 comment:

  1. na akiwa anajuana vizuri na mkubwa katika SMZ kesho tutamuona anadunda na anachukuwa rushwa tena kama kawaida, hapo atachukuliwa hatuwa mtu mburu matari tu

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.