STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 15.12.2016
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein, amemtumia salamu za rambi rambi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi
Tanzania, Jenerali Davis Adolf Mwamunyange kufutia kifo cha Brigedia Jenerali
Cyril Ivor Mhaiki, Kamanda wa Brigedia ya Nyuki Zanzibar.
Katika salamu hizo za
rambi rambi, Dk. Shein alieleza kuwa amepokea kwa huzuni kubwa taarifa ya kifo
cha Brigedia Jenerali Cyril Ivor Mhaiki, Kamanda wa Brigedia ya Nyuki Zanzibar,
kilichotokea jana katika Hospitali ya Jeshi la Wananachi wa Tanzania, Lugagalo,
Dar-es-Salaam.
Dk. Shein kwa niaba
yake binafsi pamoja na wananchi wote wa Zanzibar, alieleza kuwa wamepokea kwa
mshtuko, taarifa ya kifo cha Kamanda huyo hodari aliyetoa mchango mkubwa katika
shughuli za ulinzi na usalama na maendeleo ya nchi.
“Siku zote, Kamanda
Mhaiki alikuwa mtu mwenye mashirikiano na wenziwe, muadilifu, msikivu na mahiri
katika kazi zake”ilisema sehemu ya salamu hizo za rambi rambi.
Aidha, salamu hizo za
rambirambi zilieleza kuwa hakika Marehemu Mhaiki ameacha pengo kubwa kwa
familia yake, Brigedi ya Nyuki, Jeshi la Wananachi wa Tanzania pamoja na nchi
nzima kwa jumla huku akisisitiza kuwa mchango wake hautosahaulika.
Dk. Shein alimuomba
Jenerali Mwamunyange kuzifikisha salamu hizo za rambirambi kwa Wanafamilia,
Maofisa na Wapiganaji wa vikosi vyote vya Ulinzi na Usalama.
Pamoja na hayo, salamu
hizo zilimuomba Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira ndugu, jamaa na marafiki wa
Marehemu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huku akimuomba Mwenyezi Mungu
kumlaza mahala pema Kamanda huyo.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment