STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 23.1.2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa
mbali mbali katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Viongozi walioapishwa
na Rais Dk. Shein katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar ni Dk. Sira
Ubwa Mamboya ambaye anakuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri asiekuwa na
Wizara Maalum.
Wengine ni Bi Zainab
Omar Mohammed ambaye anakuwa Mshauri wa Rais wa Masuala ya Jamii, Wazee,
Wanawake na Watoto, Dk. Maua Abeid Daftari anakuwa Mshauri wa Rais- Pemba na Bi
Rahma Ali Khamis ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Nchi, Ofisi ya
Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
Hafla hiyo, ilihudhuriwa
na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali
Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar
Othman Makungu, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Gavu.
Viongozi wengine
waliohudhuria hafla hiyo ni Mawaziri wasio na Wizara Maalum ambao pia, ni
Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi, Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee,
Vijana, Wanawake na Watoto Shadya Mohamed Suleiman, Mufti Mkuu wa Zanzibar
Sheikh Saleh Omar Kabih, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji.
Na wengine ni Mkuu
wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed
Mahmoud, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib, Washauri
wa Rais wa Zanzibar pamoja na viongozi wengine wa Serikali.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment