Na Haji Nassor, Pemba
WIZARA ya Nchi, Afisi ya Rais,
Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, imesema iko mbioni kuandaa
sera ya utoaji wa msaada wa kisheria, kufutia haki hiyo kutolewa kwa njia ya
biashara, kama wanavyofanya baadhi ya wanasheria.
Wizara
hiyo imesema haki hiyo ambayo ni ya kikatiba, lipo kundi kubwa la wananchi
ambapo kwa unyonge wao wa kukosa fedha au uwelewa wa mambo ya kisheria, hukosa
haki zao mbele ya vyombo vya sheria, ingawa sera hiyo ikikamilika hilo
litaondoka.
Kauli
hiyo imetolewa na Afisa Mdhamini wa Wizara hiyo
Pemba Massoud Ali Mohamed, nje ya ukumbi wa kiwanda cha makonyo Wawi Chakechake, wakati akizungumza
na waandishi wa habari, mara baada ya kufungua mafunzo kwa watoa huduma za
kisheria.
Alisema
wizara imeamua kuja na sera hiyo, kwa vile wananchi wanapaswa kupata haki zao
na kujua sheria kupitia serikali yao kupitia wizara husika bila ya kujali
unyonge wao.
Hivyo
alisema lile kundi kubwa la wananchi wenye unyonge wa kifedha ua kutoweza
kujitetea mbele ya vyombo vya sheria,
sasa sera hiyo itawawezesha kuzitambua haki na wajibu wao.
“Wizara
imeona sasa kuwa, msaada wa kisheria kwa baadhi ya wanasheria wamekuwa
wakiufanya kwa njia ya kibiashara, wakati ni haki yao kikatiba, hivyo sera hiyo
ikija itatoa huduma sawa’’,alifafanua.
Akifungua
mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo watoa huduma ya msaada wa sheria kwa
wanasheria, waendesha mashitaka, mawakili, maofisa wa sheria na wasaidizi wa
sheria, Afisa Mdhamini huyo alisema mafunzo hayo, ni muhimu kwani yataibua
mbinu mpya ya kazi zao.
Mapema
wakili wa kujitegema Pemba Zaharan Mohamed Yussuf alisema changamoto kubwa
inayokabili, ni wananchi kukosa uwelewa wa kisheria na kutohifadhi kumbu kumbu
zao vyema.
Nae
msaidizi wa sheria kutoka wilaya Wete, Khamis Hamad Nassor, ameiomba jamii
kuwaamini wakati wanawapowapa masaada wa kisheria, kwani wanalengo la
kuwaelimisha haki na wajibu wao.
Mafunzo
hayo ya siku tatu ambayo yamewashirikisha washiriki 50 wakiwemo mawakili,
wanasheria, waendesha mashitaka, wasaidizi wa sheria na wadau wa sheria
yamefadhiliwa na UNDP na kutayarisha na wizara inayohusiana na katiba na
sheria.
Kituo
cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, ndio taasisi ya kwanza ya kiraia kwa
Zanzibar, kuanzisha mpango wa utoaji wa huduma za kisheria bila ya malipo,
ambapo pia mwaka 2007 ilianzisha mpango wa wasiaidizi wa sheria katika majimbo
yote ya uchaguzi Zanzibar na kwenye Idara maalum za vikosi vya SMZ kwa lengo
hilohilo.
No comments:
Post a Comment